WANANCHI WAKERWA NA MIUNDO MBINU MIBOVU HOSPITALINI
WANANCHI wa
kijiji cha Mtangani
wanaoishi karibu na
kituo cha afya
cha Bagamoyo wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba
wanalalamikia juu ya kukosekana kwa eneo malumu
la kuchomea taka za Hospitalini
hapo, jambo ambalo linaweza kupelekea kutokea kwa maradhi hatarishi ya mripuko
ikiwemo kuharisha.
Akizungumza na wandishi wa habari huko kijijini kwao Nasra Ali Makame amesema kukosekana kwa eneo
[shimo] malumu la kuchomea taka katika
kituo hicho kinawathiri, kwani wakati wa kuchomwa taka moshi husambaa kwenye makaazi yao na kusababisha
kukohoa na kupata muamsho katika miili
yao.
‘’Wanapochoma moto
taka zao, moshi na harufu yote inaingia
humu ndani mwangu, Napata muwasho mimi na watoto wangu,’’alieleza.
Faidh khamis Darusi alisema ni vyema wizara ya afya kuchukua jitihada za makusudi kuboresha miundombinu ya kuhifadhia taka kituoni hapo,ili kulinda usalama wa afya kwa watoto.
‘’Watoto na wanawake
ndio wathirika zaid, hivyo ipo haja kwa Serikali kufanya maboresho ya kuweka
eneyo malumu kwa ajili ya kuchomea taka, bila ya kuleta athiri kwa wananchi,’’alieleza.
SERA NA SHERIA.
Sera ya wizara ya Afya ya Zanzibar ya mwaka 1990 ni kuhakikisha inaimarisha huduma za
afya ya uzazi ya mama na mtoto, ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pamoja
na vya watoto wachanga.
Katika kipindi cha utekelezaji july 2022 hadi kufikia march 2023, wizara
kupitia idara ya uendeshaji na utumishi inajukumu la kuhakikisha kuwa wizara
inanyenzo ikiwa ni pamoja na rasili mali watu, fedha, majengo, usafiri na
vitendea kazi.
Comments
Post a Comment