PACSO YATAKA ASASI ZA KIRAIA KUFANYA UTETEZI WA SERA, SHERIA ZINAZO MKANDAMIZA MWANAMKE.



NA FATMA HAMAD,PEMBA

ASASI za kirai zimetakiwa kuzisemea na kuzifanyia utetezi Sera na Sheria ambazo zina mkandamiza  mwanamke na mtoto wa kike wasifikie kwenye malengo yao, ikiwemo kwenye ngazi za mamuzi.

Akiwasilisha mada mwanaharakati wa haki za binadamu kutoka [Zalho] Pemba Siti Habibu Muhamed katika mkutano wa kuibua changamoto za kisera, sharia na kanuni zinazokwaza maendeleo ya wanawake kwa asasi za kutetea haki za wanawake huko Maktaba Chake chake Pemba.

Mwanaharakati huyo alisema vipo vifungu kadhaa vya sharia vimekua vikimkandamiza mwanamke kushiriki katika sekta mbali mbali, hivyo ni vyema kusimama kidete kuleta ushawishi na utetezi, ili kuona zinafanyiwa marekebisho na mwanamke nayeye aweze kushika  nyadhifa za uongozi.

‘’Kama sisi ni wadau wa kutetea haki za wanawake, ni budi tushirikiane kwa kuzifanyia utetezi, ziweze kufanyiwa marekebisho ili kuhakikisha hazimkandamizi mwanamke na mtoto wa kike,’’ameeleza.

Alisema miongoni mwa vifungu hivyo ni kifungu cha 67 [1] cha katiba ya Zanzibar kimeleza kuwa kutakuwa na wajumbe wa baraza la wawakilishi wanawake kwa idadi ya asilimia 40 ya wajumbe wote wa kuchaguliwa kwenye majimbo ya uchaguzi.

Alifahamisha kuwa hadi sasa ni asilimia 38 tu kwenye wajumbe hao wanawake, hivyo ipo haja kwa wanaharakati kulisemea na kufanyiwa marekebisho, ili kufikia lengo la asilimia hamsini kwa hamsini  ya wanawake kwenye uongozi.

Alisema sheria nyengine ni sheria ya elimu ya mwaka 1982,  adhabu zinazotolewa kwa watoto wanaofungishwa ndoa ni ndogo,mzazi anatakiwa alipe faini isiyozidi shilingi elfu 10, na atakaposhindwa ni kifungo cha miezi 3.

‘’Tusipoipigia kelele sisi kama wadau tutaendelea kukosa viongozi wanawake  maisha yote kwenye tasisi zetu,’’ameleza.

Pia sheria ya Kadhi namba 9 ya mwaka 2017, haijangalia madhara yanayoyapatikana kutokana na kukosa mtetezi [Asesa] mwanamke kwenye mahakama hiyo.

Kwa upande wake mwanaharakati wa kutetea haki za wanawake na watoto wilaya ya Wete Sabah Mussa Said alisema utetezi na uchechemuzi wa sera unahitajika kihali na mali, kwani bado kuna watoto wenye ulemavu wamekuwa wakikosa haki zao za elimu kutokana na kukosa miundombinu rafiki maskulini, kama vile walimu mjumuishi.

‘’Licha ya kuwa Sera na Sheria ya elimu  ya mwaka 1982, imeweka mikakati kuhakikisha watoto wote wanapata elimu, lakini bado watoto wetu wenye ulemavu hawafaidiki na haki yao hiyo,’’alifahamisha.

Alieleza kuwa Skuli nyingi hazina walimu wa lugha za alama kulingana na mahitaji ya mwanafunzi, hivyo ni vyema wadau na Serikali kuliona hilo, na kuweka mazingira rafiki yatakayo wafanya nawao kuwa viongozi bora wa badae.

‘’Mimi mwenyewe Shuleni kwangu nilikua ninae mwenye ulemavu wa uziwi na mdomo, ila hakukuwa na mwalimu hata mmoja aliekua akimuelewa, tulimchukua tu ilimradi amalize tu, lakini hana alichotokanacho zaidi ya kufeli,’’alifahamisha.

Nae mkurugenzi mtendaji wa shirika la mtandao wa asasi za kiraia Pemba [Pacso] Muhamed Najim alisema lengo la mafunzo hayo kwa jumuiya hizo zinazotetea haki za wanawake, ni kujadili Sera, Sheria na kanuni ambazo zinawakwaza wanawake wasifikie malengo yao ili ziweze kujulikana na kufanyiwa marekebisho.


Katiba ya Zanzibae ya mwaka 1984 kifungu cha 6 [2] kinasema kila mzanzibar, kwa misingi ya katiba hii, ataweza kufaidi haki na fursa zote anazostahili mzanzibar.

Pia kifungu cha 12 [ 1] kinaeleza watu wote ni sawa mbele ya sharia, na wanayo haki, bila ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sharia.





 


 


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.