WASAIDIZI WA SHERIA WAHIMIZWA KUJITUMA KWA BIDII.

 

NA FATMA HAMAD PEMBA.

Jumuiya   za  wasaidizi wa  sharia  zimetakiwa  kuanzisha    miradi mbali  mbali  ya  kimaendeleo  ambayo  itawapatia    fursa   zitakazowasaidia  kupata  maslahi  katika jumuia  zao.

Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi kutoka jumuia ya wasaidizi wa sheria wa wilaya ya micheweni Moh’d Hassan Ali huko ofisi za wasaidizi wa sharia  iliyopo Wingwi Mapofu kaskazini  Pemba.

Amesema jumuiya ya wasaidizi wa sharia sio jumuia inayotengeneza kipato, lakini ni budi kuwepo na miradi ambayo itasaidia kufikia lengo la utoaji wa msaada wa kisheria kwa jamii bila ya kutegemea ufadhili.

‘’Wasaidizi wa sheria mnajukumu la kuwasaidia wananchi wakati wanapopata matatizo hivyo msikae tu mkategemea ufadhi bali na nyinyi jiongezeni ili muweze kuifikia jamii kila pembe’ alieleza mwenyekiti wa bodi.

Aidha amewataka wasaidi wa sharia kufanya kazi na vikundi vya wajasiamali  pamoja na  wafanya biashara  ili kuhakikisha nawao wanazifahamu sharia na katiba za Nchi.

‘Wapo watu wameanzisha vikundi lakini havina usajili wala katiba, hivyo ni wajibu wenu kuwafikia na kuwaelimisha jinsi ya kuviendesha vikundi hivyo’ alishauri mwenyekiti.

Mapema  msaidizi wa sharia kutoka shehia ya Tumbe magharibi Zaina Omar Othman amesema bado jamii inakabiliwa na migogoro na matatizo kadha hivyo ni wakati wasaidizi wa shria kujitoa kihali na mali  kuisaidia jamii ili kuinusuru migogoro isitokezee.

Nae kaimu mkurugenzi wa jumuia hiyo Saleh Hamad Juma  ameeleza kuwa kuwepo na mashirkiano ya pamoja kwa jumuia za wasaidizi wa sharia ni njia pekee itakayozifanya jumuia  hizo  kufikia lengo lao la  usaidizi wa kisheria. 




 

        

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.