WADAU WAOMBA SHERIA ZINAZOHUSU MASUALA YA UDHALILISHAJI ZIFANYIWE MAREKEBISHO

 


                                NA FATMA HAMAD PEMBA.

Mratibu wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa ofisi ya Pemba Fathiya Mussa Said amewataka wandishi wa habari kupaza sauti zao  kwa kuzisemea sheria mbali mbali  zenye mapungufu   ambazo zinazohusu masuala ya udhalilishaji wa kijinsia  ziweze kufanyiwa marekebisho ili zinaendana na hali ya sasa.

Mratibu huyo ameyasema hayo huko ofisini kwake  Mkanjuni Chake chake wakati akifunga mafunzo ya siku mbili  yanayohusu  mradi wa kuhamasisha hatua za kitaifa dhidi ya vitendo vya udhalilishaji Zanzibar kwa wandishi wa vyombo mbali mbali kisiwani Pemba .

Amesema licha juhudi mbali mbali zinazochukuliwa ili kuondosha udhalilishaji lakini bado kuna vifungu vya sheria vinaleta ukakasi jambo ambalo linakwaza  harakati za utetezi dhidi ya masuala hayo.

‘’Vipo vifungu mbali mbali vya sheria vinakandamiza  masuala ya udhalilishaji hivyo ni jukumu lenu wandishi wa habari kuvipiga kelele ili kuona vinarekebishwa na kuona vinaleta mabadiliko juu ya masuala haya ya  udhalilishaji’’ alieleza mratib.

Akiwasilisha mada mwanasheria kutoka Ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka [dpp] Ali Amour  Makame  amesema  miongoni mwa sheria ambazo zinavifungu vinavyoonesha mapungufu ni Sheria ya kumlinda mwari na mtoto wa mzazi mmoja, Sheria ya Ushahidi, Sheria ya mtoto, Sheria ya Jinai na Madai.

Amesema ni vyema vikangaliwa na kufanyiwa marekebisho vifungu vinavyoonyesha mapungufu  katika sheria hizo jambo ambalo litaepusha migongano katika uendeshaji wa kesi hizo.

Wakiwa katika mjadala wa pamoja wandishi waliopewa mafunzo hayo wamesema nivyema kuwepo na adhabu kali kwa pande zote mbili mke na mume wakati watakapokutwa wakifanya vitendo vya udhalilisha jambo ambalo litasaidia kupungua kwa matendo hayo.



 


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.