WASAIDIZI WA SHERIA WAWAPIGA MSASA WAZAZI



 

                     NA FATMA HAMAD PEMBA.

Jamii imekumbushwa kuacha tabia ya kuwaficha wahalifu wanaofanya vitendo vya udhalilishaji katika familia zao jambo ambalo linachangia kuongezeka kwa vitendo hivyo.

Ukumbusho huo umetolewa na msaidizi wa sharia kutoka jumuia ya wasaidizi wa sharia ya wilaya ya Micheweni Salim Hemed Salim wakati akizungumza na wananchi wa shehia ya Shumba vyamboni iliyopo wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Amesema vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto bado vinaendelea kufanyika, hivyo ni wakati wanajamii kuvunja ukimya na kuwafikisha kwenye vyombo vya sharia wahalifu wanatenda makossa haya ili kutiwa hatiani.

‘’Niwambie wazazi wenzangu kama tutaendelea kuwaficha na kuona muhali tutawafanya watoto waendelee kukumbwa na kadhya hiyo’’ alisema msaidizi wa sharia.

Mapema msaidizi wa sharia kutoka shehiya ya Shumba vyamboni Said Masoud Rashid amesema ni vyema wazazi na walezi kukaapamoja na kurudisha malezi ya pamoja katika kuwalea watoto jambo ambalo litasaidia kuondosha ushalilishaji.


Nae sheha wa shehia ya Shumba ya vyamboni Time Said Omar amevitaka vyombo vinavyosimamia sharia kutoa adhabu kali kwa yoyote atakaebainika amefanya udhalilishaji bila ya kuangalia kabila  wala cheo cha mtu.



 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.