WANDISHI WATAKIWA KUZISEMEA KERO ZINAZOKATISHA NDOTO ZA WANAWAKE, WATU WENYE ULEMAVU NA VIJANA


                                                       NA FATMA HAMAD PEMBA.

 Wandishi wa habari wametakiwa kuibua na kuzisemea kero zinazo wakabili Wanawake, Vijana pamoja na watu wenye ulemavu ambazo zinapelekea kuwakosesha fursa  mbali mbali za kimaendeleo.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa hama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa njia ya mtandao kwa wandishi wa habari wa vyombo mbali mbali kisiwani Pembakatika mafunzo ya mradi wa kuhamasisha hatua za kitaifa dhidi ya vitendo vya udhalilishaji Zanzibar .

Amesema Wandishi wa habari wanamchango mkubwa katika kuisaidia jamii kupiga hatua kimaendeleo.

Hivyo amesema kuwa wakati umefika kwa wandishi wa habari kuzisemea  kero zinazo kosesha kupata haki pamoja na fursa mbali mbali ikiwemo ya uongozi.

‘’Wandishi wa habari endeleeni kupaza sauti kwa kuzitetea hangamoto zinazowakumba wanawake, watu wenye ulemavu, Vijana ili kuona nawao wanaingia katika ngazi za maamuzi’’ alisema Bi mzuri.

Akiwasilisha mada juu ya ushiriki na ushirikishwaji wa wanawake mkufunzi wa mafunzo hayo Sabah Mussa Said watu wenye ulemavu ni kundi ambalo  maranyingi linacahwa nyuma hivyo ni vyema wandishi mkaelekeza nguvu zenu kuuelimisha umma kufahamu kwamba watu wenye ulemavu wanastahiki kupata mahitaji na fursa kama watu wengine.

Kwa upande wake mratibu wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa ofisi ya Pemba Fathiya Mussa Said amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajenga na kuwakumbusha wandishi wa habari waweze kuandika matatizo yalioyopo kwenye jamii ambayo yanawakumba wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ikiwemo usawa wa kijinsia, fursa za ushiriki na ushirikishwaji katika nafasi za uongozi, pamoja na  sheria ambazo zinamapungufu  katika maswala ya udhalilishaji.

‘’Makundi haya matatu nayo yana haki sawa kama yalivyo mengine hivyo ni wajibu wenu wandishi wa habari kwenda kuangalia ni tatizo gani linalo fanya wasifikie ndoto zao’’alieleza mratib Tamwa.

Nao baadhi ya wandishi waliopata mafunzo hayo wamesema  wakati umefika  kwa wandishi wa habari kuielimisha  jamii kuondosha  zile  itikadi potofu kwamba makundi hayo hayawezi kufanya jambo lolote lenye kuleta mabadiliko.

Mradi huo wa miaka miwili unafadhiliwa na foundation for civil society ambao unaendeshwa na Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania [TAMWA], Zafela,Tujipe na Kuhawa.

         

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.