WAZAZI WAPEWAMBINU.

 

                         NA FATMA HAMAD PEMBA.

Kukosekana  kwa  malezi  ya  pamoja  [zamani]  ni  moja  ya  sababu  inyochangia   kwa  kiasi  kikubwa kuongezeka  kwa  matendo  ya  udhalilishaji  wa  kijinsia katika jamii.

Hayo yamelezwa na mratibu wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania tamwa  ofisi ya Pemba Fathiya Mussa Said katika kongamano la madhimisho ya asasi za kiraia  ya  siku 16 ya  kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto huko micheweni mkoa wa kaskazini Pemba.

Amesema licha ya elimu inayotolewa juu ya udhalilishaji lakini bado  suala hilo  linazidi kuongezeka hivyo wakati umefika kwa wazazi kukachini  ili kurudisha malezi ya zamani hali ambayo itakua ni muarubaini wa hayo.

‘’kwa kweli hali imekua tete  jamani suala la kukaa kila mtu na mwanawe imeshapitwa na wakati tukaeni tutafakari ni hatari sana’’ alieleza kwa masikitiko mratibu tamwa.

Kwa upande wake afisa dawati la jinsia la wanawake na watoto wilaya ya micheweni Mohamed Ali ameitaka jamii  kuanzisha kamati za madili katika shehia zao na kujiwekea sheria ndogo ndogo ambazozitawachukulia hatua wale wote watakaobainika wanajihusisha na vitendo viovu.


Nae makamo mkurugenzi  wa jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya micheweni Saleh  Hamad  Juma amesema ili kumaliza udhalilishaji ni vyema  kila mmoja kwa nafasi yake kufanya kazi kwa madili ya kazi yake  ili kuepusha  malalamiko  ya wananchi.


Nao wasaidizi wa sheria wilaya ya Micheweni wamevitaka vyombo vinavyoshuhulikia kesi za udhalilishaji kuzichunguza na kufanya upelelezi  wa hali ya juu dhidi ya kesi hizo kwani kumekuwepo na baadhi ya wazazi huwafanya mabinti zao kama ni kitega uchumi na kuwabambikizia kesi wenziwao.

Kongamano hilo ni shamra shamra ya mishimisho ya siku 16 ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto.


 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.