WAZAZI WANYOOSHEWA VIDOLE

 









                  NA FATMA HAMAD PEMBA.

Wazazi na walezi wamenyoshewa kidole kwamba nawao ni moja ya chanzo kinachopelekea  vijana kujiingiza katika matendo     vya udhalilishaji wa kijinsia.

Wakizungumza katika kongamano la maadhimisho ya asasi za kirai  la siku 16 za kupinga ukatili wa wanawake na watoto wanafunzi wa  skuli ya msingi mitiula wete Pemba wamesema wazazi wamekua hawana tabia za kufuatilia nyenendo za watoto wao wakati wanapotoka kwenda madrasa pamoja na shuleni.

Wamesema wapo baadhi ya wanafunzi wanatabia wanapondoka skuli hawafiki majumbani kwao wanaishia vichochoroni hivyo  wazazi  kuweni makini juu ya watoto wenu msiwachie fursa mpaka wakajisahau.

‘’Unapotoka nyumbani  mzazi hakuulizi  unakwenda wapi na wala unarudi mda gani  yani mda wako mwenyeo tu na safari zako hakuna wa kukubugudhi’’ walisema wanafunzi.

Bimkubwa Issa Omar mwanafunzi kutoka chuo cha afya wete amesema Kuwepo kwa masomo ya ziada yasiyo na mpangilio yanachangia watoto kufanyiwa udhalilishaji.

‘’Sikuhizi  mpaka wa watoto wa cheke chea na darasa la tatu wanakwenda masomo ya ziada je tunawalinda vipi humo njiani wanamopita hebu tuliangalieni hili jamani’’alisema Bimkubwa.

Akifungua kongamano hilo katibu tawala  wilaya ndogo Kojani Makame Khamis amesema udhalilishaji hautondoka kwani bado  wazazi hawajakua imara na imani thabit katika malezi ya watoto wao.

‘’Wazazi tukataka tusitake hatujakuwa na ikhlasi katika malezi mtu akishapeleka mapembe na samaki aona ndo kazi imekwisha sivyo hivyo watoto wetu wanapotea’’ alisema katibu tawala.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.