WANAFUNZI WAPEWA MBINU ZA KUDHIBITI UDHALILISHAJI

 

NA FATMA HAMAD PEMBA.

Wanafunzi   maskulini  wameaswa  kuepuka   kufanya  vitendo  vya  utovu wa nidhamu na badala yake wafuatilie masomo yao kwanza  ili waweze kufikia  katika  ndoto  zao.

Hayo yamesemwa na  Afisa dawati wa jeshi la Polisi  wilaya ya Micheweni Mohd Ali wakati akizungumza na wanafunzi wa almadrasatul madyana imuslimina  iliyopo wingwi mtemani wilaya ya micheweni Kaskazini Pemba.

Amesema kesi nyingi zinazoripotiwa zaidi  ni  za  watoto  kuanzia  miaka 14 hadi 16 jambo ambalo linapelekea kukosa kuendelea na masomo yao.

‘’Sasahivi ni wakati wa kusoma  tu nyinyi  msikubali kushawishika  mkajingiza kwenye starehe mtakosa haki zenu za elimu’’ alieleza afisa dawati.

Kwa upande wake msaidizi wa sheria shehiya ya Micheweni  Riziki Ali Hamad amewataka wanafunzi hao kutoa tarifa kwa walimu wao ama wazazo wao wakati watakapoona kunakuwepo na viashiria vinavyopelekea udhalilishaji ili  viweze kuchukualiwa hatua  za kisheria  jambo ambalo lipawaepusha  na vitendo hivyo.

‘’ikiwa mnafanyiwa vitendo vibaya msikae msikae kimya toweni tarifa  hata kama ni mwalimu wako mkuu basi semeni miogope’’ alieleza bi riziki.

Nao baadhi ya walimu wa madrasa hiyo wamesema ni vyema Serikali ikangalia tena kwa umakini sheria ya mtoto ili kuona  adhabu inatolewa kwa wote wawili mwanamme na mwanake  kwani  sasahivi watoto wa kike  wanajifanya kama ni biashara.

Elimu hiyo iliyotolewa madrasani hapo ni shamra shamra ya maaadhimisho ya siku 16 za kupinga udhalilishaji kwa wanawake na watoto.

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.