JUMUIA YA WATU WASIONA [ZANAB] PEMBA WAOMBA MSAADA



 

NA FATMA HAMAD PEMBA.

Jumuia ya watu wasiona [Zanab ] wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba imeitaka Serikali pamoja na watu wenye uwezo kuwapa msaada wa  kuwajengea jingo la Ofisi yao ili kuwaondoshea usumbufu kwa wanajumuia hao.

Akizungumza na mwandishi wa habari mwenyekiti wa jumuia hiyo Suleimana Mansour Suleiman huko ofisini kwake Chake chake Pemba amesema  wanachangamoto kubwa ya uhaba wa vyumba katika jingo lao.

Amesema Ofisi yao inawafanyakazi  mchanganyiko wa watu tofauti wakiwemo watu wenye ulemavu wa Ngozi, wenye ulemavu wa viungo na  wasiona  lakini wanachumba kimoja tu hawana sehemu nyengine  ya kufanyia shuhuli zao za kiofisi.

Amefafanua kuwa unapofika wakati wa sala wanalazika wengine kukaa nje na kupishana  kwa ajili ya kutekeleza ibada ya sala.

 ‘’Jengo letu ni dhaifu, Tunachumba kimoja tu hatuna hata chumba cha stara, ukiangalia tupo mchanganyiko wanawake na wanaume’’, Alisema

mwenyekiti.

Samba mba na hilo mwenyekiti huyo ameeleza kwa masikitiko  makubwa wanakabiliwa na changamoto  ya ukosefu ya huduma ya choo katika ofisi yao.

Amesema wanalazimika kutumia huduma ya vyoo vya jirani wakati wanapokwenda kufanya haja zao hali ambayo inapelekea  wafanyakazi wake kushindwa  kuhudhuria kazini kwa wakati.

Tunakwenda choo cha Mkuu wa wilaya, Hospital na ikitokezea wenyewe ikiwa hawapo  kazini tunahangaika hatuna pakujisaidia, hivyo tunaomba msaada tujengewe japo vyumba viwili tu.

‘’Ivi Serikali sisi watu wenye ulemavu haituoni tumekosa nini sisi,ata pakwenda haja ndogo hatuna’’ Alisema mwenyekiti wa Zanab.

Mapema Mratibu wa Idara ya watu wenye ulemavu Pemba Mashavu Juma Mabrouk amesema atafanya jitihada ya kuwasaidia walemavu hao ili waweze kuondokana na changamoto hiyo.



Mkuu wa wilaya ya Chake chake Abdala Rashid Ali  amefahamisha kuwa ofisi yake iko kwenye harakati za kutafuta msaada mbalilimbali japo kwa  wahisani  wengine kuhakikisha wamejengewa majengo ili kuona kilio cha  walemavu hao kimepatiwa ufumbuzi.

‘’Ni kweli ofisi hiyo inachangamoto ya majengo pamoja na choo,ila tunawaomba wavute subra  tupo mbioni kulitafutia ufumbuzi,’’ Alisema mkuu wa wilaya.

 

 

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.