WANDISHI WAONYWA KUEPUKA KUANDIKA HABARI ZA UCHOCHEZI


 Wandishi wa habari wametakiwa kuepuka kuandika habari zisizo na mizania na zenye viashiria vya uchochezi ili kusaidia kuepusha  kutokea  kwa  migogoro isiyo ya lazima katika jamii.

Wito huo ulitolewa wakati wa mafunzo ya kujenga amani na utatuzi wa migogo kwa waandishi wa habari kisiwani Pemba yalioendeshwa na shirika la kimataifa la utatuzi wa migogor la SEARCH FOR COMAN GROUND kupitia mradi wa Dumisha amani Zanzibar.

Akizungumza na wandishi wa habari katika mafunzo  ya kutatua migogoro kwa njia shirikishi yenye lengo la kudumisha amani Husein Faraji Sengu amesema lengo la mradi ni kusadia kutatua migogoro ya kisiasa hususani mara baada ya kumalizika uchaguzi Zanzibar.

Amesema uzoefu unaonyesha kua Zanzibar mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi kumekua kukitokea athari nyingi za kisisiasa ambazo zinatokana na uchaguzi ikiwemo migogoro kwa matabaka tofauti ambayo ikiachiwa iendelee inaweza kuondosha amani ya zanziba iliopo.

Amesema wakati mwengine vyombo vya habari vimekua vikinyooshewa vidole ndio  kusababisha kuchochoa au kukuza mizozo inayo tokea katika jamii kutokana na kuhabarisha visivo sahihi ikiwemo kuandika kwa kuegea upande mmoja.

Amesema uandishi wa habari wa namna kama hiyo unasababisha jamii kukosa imani na muandishi na chombo chake cha habari sambamba  Nchi kuingia katika migogoro, hivyo amesema niwakati sasa waandishi kubadilika na kuweka umakini wa  hali ya juu  wakati wa kuandika na kuripoti taarifa.

Amesema ni vyema kwa wandishi wa habari kutumia kwa uweledi ujuzi wao na kuzingatia madili ya habari wakati wanapokua katika majukumu yao ili kuona wanandika habari zenye ukweli na zenye kuleta mabadiliko chanya kwa jamii na nchi.

‘’Wandishi wa habari acheni kuandika habari zisizo zingatia maadili ya habari, epukeni kuandika habari zenye uchochezi ambazo hazina maslahi kwa umma’’, Alisema Meneja.

Haji Nassor Mohd kutoka mtandao wa pemba to day ambae ni miongoni mwa wandishi walioshiriki mafunzo hayo amewataka wandishi wenzake kuyatumia vyema mafunzo katika kuandika habari  ili kuona  wanaleta mabadiko sahihi ndanin ya jamii.



Aidha waandishi wengine waliofaidika mafunzo hayo ikiwa ni pamoja na Mwamize Moh’d Nao  wameahidi kuyatumia na kuifanyia kazi taaluma walioipata ili kuona wanandika habari bila ya kuegemea upande wowote.


Mafunzo hayo ya siku 3 yaliojumuisha wandishi wa vyombo mbali mbali kisiwani pemba yameandaliwa na Seach for Comman Ground kwa kushirikiana na the fondation  fo civil Socity chini  ya ufadhili wa  Uropean Unian.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.