JESHI LA POLISI LA DAIWA KUFANYA SULUHU KESI ZA UDHALILISHAJI



 NA FATMA HAMAD PEMBA.

Wadau wa kupinga ukatili na  udhalilishaji wa kijinsia kisiwani Pemba wamelalamikia juu ya uwepo  wa baadhi ya Askari wanaozifanyia suluhu kesi za udhalilishaji.

Akizungumza katika mkutano wa uwasilishaji wa ripoti  ya utekelezaji wa mradi  wa kuchukua hatua dhidi ya vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia  msaidizi wa sheria kutoa mkanyageni mkoani pemba Shaban Juma Kassim huko ofisi za chama cha Wandishi wa habari Wanawake Tanzania [TAMWA]  Chake chake  amesema kazi ya askari ni kufanya upelelezi tu na sio kutoa suluhu.

Amesema wapo baadhi ya askari huwataka wazazi wanaokwenda  kuripoti kesi za udhalilishaji kuzimalizia vituoni tu na wasiende mahakamani.

‘’Bado wenzetu wa Jeshi la polisi wanaturejesha nyuma hawajakuwa tayari kukomesha udhalilishaji,’’Alisema msaidizi wa sheria.

Hivyo amewataka wazazi wa wathirika wa matukio hayo wasikubali suluhu bali wasimame kidete kutoa ushahidi ili kuona kesi zao zimepatiwa hatiani.



Kwa upande wake Haji Shoka Khamis msaidi wa sheria kutoka Chokocho amesema udhalilishaji utaendelea kuwakumba wanajamii kwani bado hakuja kuwepo na sauti ya pamoja [mashirikiano] kati ya Wananchi, Wadau wa kupinga udhalilishaji pamoja na taasisi za kisheria ikiwemo Jeshi la Polisi.

Baadhi ya wazazi wa wathirika wa udhalilishaji walioshiriki mkutano huo wamesema bado kumekuwepo na udhoroteshwaji wa uwendeshwaji wa kesi mahakamani jambo ambalo linawafanya wananchi walio wengi kushindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi.

‘’Tunaumia jamani mtu anatoka muambe anakuja chake, akifika anambiwa mjoo kesho mjo kesho kutwa  tunaumia hatuna nauli tuwanyonge,’’ Alidai mzazi.

Mapema mrajis wa mahakama kuu Chake chake Abdul razzak Abdul kadir Ali amesema wengi wanaofanyiwa matendo hayo ni watoto kuanzia mika 18 hadi 15 ambapo tayari wameshajielewa, hivyo amewataka wazazi kuweka utaratibu kama vile zamani wa kuwapekuwa watoto wao wakati wanaporudi safari zao, kwani kufanya hivyo kutawatia hofu na kujiepusha kufanya matendo maovu.



Nae mratibu wa chama wa wandishi wa habari Wanawake Tanzabia [TAMWA ofisi ya Pemba Fathiya Mussa Said amewapongeza wadau hao kwa kazi kubwa walioifanya juu ya ufuatiliaji wa kesi hizo, hivyo amewataka kuongeza nguvu ya mapambano ili kuona udhalilishaji umendoka na jamii kubaki salama.



 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.