ZAEKA YATAKIWAN KUHAMIA KATIKA OFISI ZA VYAMA VYA SIASA WAKATI UNAPOFIKIA KIPINDI CHA CHAGUZI


                        NA FATMA HAMAD FAKI MPEMBA.

Mamlaka ya kuzuia Rushwa na uhujumu uchumi Zanzibar [ZAEKA] imetakiwa kuelekeza nguvu zao za uchunguzi  katika vyama vya siasa wakati unapofikia uchaguzi mkuu wa Zanzibar ili kuwakamata na kuwachukulia hatua wale ambao watabainika kutoa rushwa kwa ajili ya kupata nafasi za uongozi Majimboni.

Wito huo umetolewa na baadhi ya Wanawake waliogombea nafasi mbali mbali za uongozi katika uchaguzi mkuu uliopita  2020 wamesema wakati unapofika kipindi cha uchaguzi rushwa imekua ikitawala kwa kiasi kikubwa katika vyama siasa nchini.

Wamefahamisha kuwa nafasi za uongozi majimboni asilimia kubwa huchukuliwa na wale wenye pesa tu, jambo ambalo linawakatisha tama wanawake masikini wenye nia ya kugombea kushindwa kuwania  nafasi hizo.

‘’Tuna iomba  zaeka  itende haki, katika kazi yao ya kupambana  na rushwa na uhujumu uchumi kuwachukulia hatua wale wote ambao wanatumia nguvu ya fedha kama njia ya kupata madaraka,’’ Walisema wanawake wagombea.

Aidha wamesema endapo kwa viongozi wa vyama vya siasa hawatobadilika na kuliondosha suala la rushwa kutakuja  kukosekana kwa viongozi wanawake majimboni hususan wenye uwezo mdogo wa kifedha.

Mratibu chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania [TAMWA] ofisi ya Pemba  Fathiya Mussa Said amesema kuwepo kwa rushwa katika chaguzi kunapelekea kukosekana kwa viongozi wadilifu na wawajibikaji kwa wananchi, hivyo amewataka viongozi wa vyama vya siasa kutoa fursa  kwa wale wagombea ambao wanakubalika na jamii  na sio  tu kwa wenye uwezo wa kifedha.

 ‘’Wito wetu sisi chama cha wandishi wa habari wanawake Pemba tunavishauri vyama vya siasa kutoa fursa kwa wagombea ambao wanakubalika na Jamii’’, Alisema mratibu Tamwa.


Baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa  wakiwemo CCM NA ACT Wazalendo wamesema rushwa ya ngono ndio iliyokua ikidaiwa katika vyama vyao, ila kwasa  suala hilo limeondoka, kwani Serikali imeweka mkakati madhubuti wa kuwachukulia hatua kali za kisheria watakao bainika wanajishuhulisha na masuala hayo.



Nae Afisa wa mamlaka ya kuzuia rushwa na uhujumu uchumi Zanzibar Zaeka Kisiwani Pemba Suleiman Ame Juma  amesema rushwa si katika chaguzi tu, hivyo amewataka wagombea wanawake kushirikiana na mamlaka hiyo kutoa ushahidi ili kuwakamata wale wote wanaofanya matendo hayo.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.