SHAHIDI APELEKEA KESI KUGHAIRISHWA.
Kutokuwepo kwa shahidi
kumesababisha hakimu wa Mahakama ya Mkoa B iliopo Chake chake kughairisha kesi ya
kuingilia kinyume na maumbile inayomkabili kijana Ayoub Mohd Hamad mwenye umri
wa 18 mkaazi wa Likoni kengeja Wilaya ya Mkoani Pemba.
Baada ya mtuhumiwa huyo
kupanda kizimbani akisubiri kusomewa shitaka lake, Wakili wa Serikali kutoka
Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka [DPP] Ali Amour Makame amesema leo walikua wasikilize shahidi ambae ni askari mpelelezi ila
hakufika mahakamani kwani hayupo kazini yupo likizo.
‘’Mheshimiwa hakimu tunaomba uipangie sikunyengine ili
tumuombe shahidi wetu aje kutoa ushahidi
hata kama amesafiri,’’ Alidai DPP.
Hakimu wa mahakama hiyo Lusiano makoe nyengo amekubaliana na ombi hilo na kesi hiyo itaendelea tena tarehe 26/7/mwaka huu.
Imedaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo siku ya tarehe 23/2/2021 majira ya 5;30 asubuhi, huko Likoni Kengeja wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba Alimuingilia kinyume na maumbile ambapo kufanya hivyo ni kosa kinyume na kifu cha 133 [a] cha sheria ya adhabu sheria nambari 6 ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar.
Comments
Post a Comment