FAMILIA YA AHMED AL FARSII KUTOKA DUBAI YA HIDI KUSAIDIA VIFAA VYA TIBA HOSPITALINI





NA FATMA HAMAD PEMBA.

Ugeni kutoka falme za kiarabu [Dubai] umeahidi kusaidi  vifaa vya  tiba kama vile vya upasuaji, usafishaji wa figo,  Exray, vifaa vya uchuguzi wa magonjwa ya akinamama na watoto, na huduma nyengine mbali mbali za matibabu katika hospitali za Wilaya Kisiwani Pemba.

 Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui   amesema ahadi hiyo imefuatia ziara ya kutembelea hospitali hizo iliyofanywa kati ya uongozi wa wizara ya afya  na Ugeni huo  kujionea hali halisi ya utoaji wa huduma za afya katika hospitali ya  Wete,  Micheweni na Vitongoji pamoja na kusikiliza changamoto zilizopo.

 Amesema baada ya kuwatembeza na kujionea katika hospitali hizo, Ugeni huo umejionea mahitaji ambayo yanahitajika ambapo wameyachukua na kwenda kuyafanyia kazi pamoja na  kuahidi kurudi baada ya miezi michache nayale ambayo yatashindwa kutekelezwa na ugeni huo wataangalia namna ya kuomba msaada kwa wahisani wengine.

 ‘’Atahakikisha ametekeleza ahadi aliyoiweka japo kuomba misaada kwa wahisani wengine’’ Amesema Mazrui.

 Ameeleza kuwa lengo la ugeni huo ni kuwasaidia wazanzibar katika masuala ya afya, hivyo ameitaka Wizara ya Afya kumpa mashirikiano ili kuona alilolikusudia limefanikiwa kwa maslahi ya Wananchi.

 

 Akizungumza  Ndugu Ahmed Alfrsy ambaye aliongozana familia yake katika ziara hiyo amesema lengo ni kusaidia kutatua changomoto ya vifaa vya tiba kwenye hospitali hizo ili huduma ziweze kupatikana kwa wepesi bila ya kutumia gharama kubwa ambapo wengine wanashindwa kuzimudu.



 Mmoja kati ya madaktari dhamana  kisiwani Pemba Dr. Sharriff  Hamad Khatib kutoka hospitali ya Vitongoji amesema wana imani kubwa na ujio wa ugeni huo kwa vile umeahidi kusaidia upatikanaji wa vifaa muhimu vya kutolea huduma katika hospitali zao.

 Katika Ziara hiyo ya Siku moja ugeni huo ulipata kutembelea hospitali za Vitongoji na Micheweni Cottage na Hospitali ya Wete sambamba na kutembelea kwenye kijiji cha Shumba Mjini.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.