RUSHWA MUHALI BADO NI GUMZO KWA KESI ZA UDHALILISHAJI

 

                         NA FATMA HAMAD PEMBA.

Kuepo  kwa rushwa muhali katika jamii bado ni  changamoto  kubwa  inayopelekea kukwamisha  kwa kesi za udhalilishaji zisipate hatia.

Akitoa ripoti  juu ya kesi za udhalilishaji mwendesha mashtaka wa serikali kutoka oisi ya mkurugenzi wa mashtaka  Chake  chake  Mussa Khamis katika kikao cha kamati ya kupinga udhalilishaji kilichofanyika ofisi za Tamwa Kisiwani Pemba.

Amesema licha ya elimu inayotolewa kwa jamii ili kuacha muhali lakini bado hawaja kuwa tayari juu ya mapambano dhidi ya udhalilishaji.

‘’Bila ya mashirikiano ya pamoja hatuwezi tukafika pahala jamani tutabakia tunaimba tu  kila siku alisema PP Mussa.

Aidha kwa upande mwengine alifahamisha kuwa kesi zinazowapa  changamoto katika uwendeshaji wake ni za watoto wa miaka 15, 16 na 17 hawataki kutoa ushirikiano  mahakamani.

Baadhi ya wanakamati hiyo kutoka wilaya ya Mkoani wamekua wakivilalamikia vituo vya Polisi Mtambile na kengeja kuwa bado havijakuwa makini kudhibiti vitendo ya udhalilishaji.

‘’Sisi tunashangaa kesi zinazoripotiwa vituoni humo watuhumiwa wengi wanakimbi inakuwaje wasikamatwe’’ alisema Haji shoka kutoka mkoani.

Nae mratibu wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa upande wa Pemba Fathiya Mussa Said amewataka wanamtandao hao kuendelea kuchukua jitihada za makusudi kuwaelimisha wanajamii kutoa tarifa mapema wakati unapotokezea udhalilishaji samba mba na kuika mahakamani kutoa ushahidi.

Jumla ya majalada 66  ya udhalilishaji yalipokelewa katika ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka DPP  mkoa wa kusini Pemba ambapo  majalada 37  yalifunguliwa mahakamani, 21 yanaendelea na upelelezi na 8  yaliffungwa kutoakana na sababu za kiushahidi kwa kipindi cha Januari hadi  june mwaka huu.

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.