Wananchi nendeni mkaripoti kero zenu


 

                               NA FATMA HAMAD PEMBA.

Mkuu wa wilaya ya  Wete Hamad Omar Hamad amewataka wananchi wa mkoa wa Kaskazini Pemba kujitokeza kwa wingi katika kambi ya utoaji wa huduma ya Msaada wa kisheria ili waweze kupeleka matatizo yao na kupatiwa ufumbuzi.

Mkuu huyo ameyasema hayo huko Micheweni wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya  Msaada wa kisheria ya Mama Samia kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud amesema Kambi hiyo ya siku tatu itawasaidia Wananchi kupata huduma na pia kujua wapi waripoti malalamiko yao.

Amesema Jamii imekua ikikabiliwa na matatizo mbali mbali ikiwemo ya Ndoa, Ardhi,Mirathi, na Udhalilishaji hivyo ni wakati wananchi kuitumia fursa hiyo ili kuweza kupatiwa msada wa kisheria.

‘’Kambi hiyo itajumuisha Wanasheria, watoa huduma ya msaada wa kisheria hivyo tuwatumieni  kwani ni bure hakuna malipo yoyote,’’alisema.

Kwa upande mwengine Hamad amewataka Wandishiwa Habari kutumia kalamu zao kwa kuwafahamisha wananchi ili waweze kufahamu na kujitokeza kwenye kambi hiyo.


Mapema akitoa salamu kutoka UN WOMEN Recho Goma amesema takriban wanawake Bilioni 2.5  dunia wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma za kisheria.

Amesema uwepo wa Mswaada  wa kisheria ni suala mtambuka kwani kutasaidia upatikanaji wa huduma za kisheria kwa Jamii.


Afisa mdhamini wizara ya Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala bora Halima Khamis Ali amesema wameamua kueka kambi hiyo Micheweni kwa makusudi ili kuona wananchi wasio na uwezo na wao wanafaidika msaada huo.

‘’Tunafahamu kuna watu hawajui hata pakukimbilia wala pakuanzia wakiwa na matatizo, hivyo kambi ii itakuwa ni Faraja kwao,’’ anasema.


Nae Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Hanifa Ramadhan Said amesema lengo la kampeni hiyo  ni kuona kila mwananchi anapata haki ya sheria.

‘’Hakuna kuachwa mtu nyuma tutahakikisha kila mzanzibari anapata haki ya kisheria na anazimtambua sheria,ameeleza.



Kambi hiyo ya utoaji wa huduma ya Msaada wa kisheria imenza October 17  hadi 19, ambapo Wanasheria, Pamoja na Mamlaka zote zinazohusika na masuala ya kisheria watapatikana katika kambi hiyo.

 


Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO