Wanaume msizitelekeze familia zenu

 

NA FATMA HAMAD, PEMBA,

Afisa mdhamini Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Hafidh Ali Mohamed amewahimiza wazazi hussusan wa kiume kusimamia majukumu yao ya kutunza na kulea familia zao ili kuwalinda watoto na vitendo viovu ikiwemo udhalilishaji na ujambazi.

Afisa huyo ametoa wito huo wakati akifungua mafunzo ya siku moja yanayohusu kuwashirikisha wanaume katika malezi kwa Wasaidizi wa Sheria huko Makonyo Chake chake Pemba.

Alisema wanaume ndio wenye jukumu  kubwa  la kuhudumia familia zao, hivyo endapo hawatofuata vyema  wajibu wao huo kutapelekea kupatikana kwa watoto wa mtaani pamoja na udhalilishaji kwa watoto.

‘’Niwasihi wazazi wenzangu wa kiume sisi ndio wenye dhamana za kutoa matunzo, hivyo tusizitelekeze familia zetu tutasababisha matatizo,’’alisema mdhamin.

Aidha aliendelea kuwasihi wazazi kuwa na subra katika ndoa zao ili kuepusha talaka, kwani hilo ni moja ya sababu inayochangia watoto kudhalilishwa.

‘’Watoto wengi wanaokosa malezi ya pamoja ya Baba na Mama mara nyingi hukosa haki zao ikiwemo Elimu pamoja na matunzo,na mwisho wa siku hupata udhalilishaji,’’alieleza.

Mapema Afisa mdhamini wizara ya Katiba, Sheria na Utawala bora Halima Ali Khamis aliwataka Wasaidizi wa Sheria kuendelea kuielimisha Jamii kulea woto wao katika malezi ya pamoja ili kuweze kupatikana kwa kizazi chenye maadili mema.

‘’Jamani kwa kweli hali ni mbaya, tuifahamisheni jamii kwamba mtoto asiwe wa mtu mmoja tu bali alelewe na jamii huenda yakapungua hayo matendo maovu vijijini mwetu,’’alisisitiza.

Aidha aliendelea kusema kuwa vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia bado vinaendelea kutokea katika jamii, hivyo wasaidizi wa Sheria mnadhima kubwa ya kuielimisha Wananchi kuongeza kasi ya kupiga ita matendo hayo.

‘’Jamani tusidharau vitendo vya udhalilishaji bado vipo,tuendeni kutoa elimu ili jamii ichukuwe tahadhari ili tujikinge navyoalieleza,’’Halima.

Kwa upande upande wake Mkurugenzi Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Hanifa alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uelewa wasaidizi wa Sheria ili waweze kuielimisha Jamii kusimamia vyema majukumu ya familia zao.

Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamesema ipo haja kwa wasaidizi wa Sheria kufundishwa lugha za alama, jambo litalopelekea watu wenye ulemavu nawao kupata haki ya msada wa kisheria pindi wakikutwa na matatizo.

Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’

UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI