Vijana Pemba waliojiajiri ufugaji Kaa wasahau ajira ya Serikali
NA FATMA
HAMAD PEMBA,
Vijana
wameonywa kuepuka kukaa katika vigenge viovu ,na badala yake
wajiunge na vikundi vya ushirika, ili waweze
kujipatia kipato cha halali.
Ushauri huo umetolewa na
katibu wa kikundi cha ushirika mapambano coperetive kinacho
jishuhulisha na ufugaji wa Samaki, kaa, kamba na mboga
mboga Bishara Muhammed Musa mbele ya wanakikundi
hao, mara baada ya kuzungumza na mwandishi wa habari huko kikunduni
kwao Sizini wilaya ya Micheweni Pemba.
Alisema wakati
umefika kwa vijana kuwamka na kujiajiri wenyewe, na sio
kukaa tu vigengeni na kusubiri ajira Serikalini.
‘’Vijana mtakapo
jiajiri mtaepukana na vitendo vya wizi, ubakaji na ujambazi,’’
alishauri katibu.
Aidha alieleza
kuwa sera ya Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ya uchumi
wa buluu unaelekeza zaidi kwenye bahari,
hivvyo aliwasisitiza viajana
hao kukiendeleza kikundi chao kwa juhudi zote, jambo ambalo
litawawezesha kupata ursa mbali mbali za kimaendeleo.
Mapema mwanakikundi Khadija Ali Juma alieleza kuwa ameamua kujiunga kwenye kikundi cha ujasiriamali, ili aweze kujipatia kipato kitakacho msaidia katika familia yake.
Aidha alisema mafanikio
hayaji tu kama ndoto, hivyo ni vyema kuwa wavumilivu kupitia changamoto
zinazowatokezea ili waweze kukiikisha mbele kikundi chao.
Akieleza changamoto
zinazowakwaza kikundi hapo ni vitendea kazi,
ikiwemo maberi pamoja mapauro.
Mwenyye kiti wa kikundi hicho Khalfan Hamad Khalfan alieleza kuwa matarajio yao ni kuhakikisha wamekuwa wazalishaji wakubwa wa mazao ya baharini.
‘’Tunatarajia
kuzalisha Tani moja ya kaa, na Tani moja ya
Kamba kila baada ya miezi miwili, na tani moja ya Samaki ndani ya
kipindi cha mwaka mmoja,’’ alisema mwenyekiti.
Hivyo aliomba wizara ya
uchumi wa buluu kujitokeza na kuwaunga mkono vikundi ambavyo vimewekeza juhudi
zao kwenye maeneo ya bahari, ili waweze kunufaika na fursa
zilizomo, ndani ya sera ya uchumi wa buluu.
Nae afisa kutoka wizara ya uchumi wa buluu Pemba Mohd Ali aliwapongeza Vijana hao kwa kuondosha dhana ya kusubiri ajira Serikali na kuamua kujiajiri wenyewe.
Aliendelea kusema
Serikali haina uwezo wa kuajiri watu wote, hivyo ni vyema vijana kuiga mfano wa
wenzao hao kwa kujiajiri ili waweze kujipatia kipato cha halali sambamba na
kuondokana na Umaskini uliokithi.
MWISHO.




Comments
Post a Comment