JAMII YAHIMIZWA KUITUNZA AMANI ILIYOPO NCHINI
Viongozi wa
kamati za dini mbali mbali kisiwani
Pemba (Pemba Interfaith Committee) wameipongeza jamii ya wazanzibari kwa kuendelea kuishi kwa umoja na
mshikamano, jambo lililoifanya Zanzibar kua mfano bora wa ustaarabu na utulivu.
Akitoa
tamko la kamati hiyo katika kikao cha kufanya tathmini ya juhudi zilizofanywa
na kamati hiyo za kushajihisha amani
kabla, wakati na baadhi ya uchaguzi mkuu uliofanyika Zanzibar mwenzi Oktaba
mwaka huu, Mwenyekiti wa kamati ya dini mbali mbali kwa upande wa wanawake
Amina Salim Ahmed katika ukumbi wa
mikutano wa Samail Gombani Pemba aliipongeza jamii ya kwa kuendelea kuishi kwa
umoja na mshikamano jambo lililoifanya zanzibar kua mfano bora wa ustaarabu.
Alisema
hali hiyo ilikuja kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa na viongozi wa dini,
Serikali, na wananchi katika kudumisha misingi ya maelewano ambayo imeijenga
Zanzibar.
Alieleza
tamko hili ni mwendelezo wa wito wa kila mara unaosisitiza kwamba amani
tulionayo ni tunu na kial mmoja anapaswa kuithamini na kuilinda kwa matendo ya
kheri na kauli zenye hekima.
Alifafanua
kua dini zote upendo, ustahamilivu, na kuheshimu utu wa kila mwanadamu, hivyo
ni vyema kila mmoja kuendeleza kuyaishi mafunzo haya katika maisha ya kila
siku.
"Dini
zote zinafundisha upendo, ustahamilivu na kuheshimu utu wa kila mmoja, hivyo ni
vizuri muendelee kuyaishi mafunzo haya katika maisha ya kila siku"
alieleza.
Aidha
aliendelea kusisitiza juu ya umuhimu wa kuendelea kutumia marifa, busara na
subira katika kushughulikia mambo mbali mbali ya kijamii na kifamilia ili
kudumisha amani iliopo katika visiwa vya Zanzibar.
Aidha
alisisitiza matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii ikiwa ni pamoja na
kuelimishana na kuhamasishana mambo yenye faida kwa jamii pamoja na kuepuka taarifa zisizo za msingi au
kauli zinazoweza kupunguza heshima baina ya watu.
Aidha
taasisi hiyo ilitoa shukrani kwa taasisi zote zinazounga mkono juhudi za kukuza
amani, kujenga uwezo wa vijana na kuimarisha huduma za kijamii.
Awali akiizungumza katika mkutano huo Mratibu Ofisi
ya Mufti Pemba Said Ahmad Mohamed aliwataka wajumbe wa kamati hiyo kuendelea
kuhubiri amani katika maeneo yao, pamoja na kutoa taarifa za viashiria vya
uvunjifu wa amani katika vyombo vya sheria.
"Endeleeni
kuhubiri amani katika maeneo yenu kwa kutumia njia mbali mbali ili kuhakikisha
amani iliopo inadumu toeni taarifa ya viashiria vya kuvunjwa kwake katika
vyombo vya sheria ili hatua ziweze kuchukuliwa, " alieleza.
Akizungumza
kwa niaba ya wajumbe wa kamati hiyo Fadhil Juma Mohamed Naibu katibu wa Jumuiya ya walimu wa Madrasa
Pemba alisema, wamekua wakifanya juhudi mbali mbali za kuelimisha jamii kwa
kuwafikia watu wa makundi mbali mbali wakiwemo vijana na wanawake katiika
kulinda amani kwa kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani katika kipindi
chote cha uchaguzi mpaka kumalizika kwake.
Aidha
waliahidi kuendeleza kutoa elimu hiyo kwa kila kundi lililopo katika jamii zao,
ili kuona Zanzibar inaendelea kudumumu katika amani kwa maslahi ya nchi.
Kwa
upande wake Afisa Mradi wa Swahili Coast wa kamati hiyo Khelef Nassor Rashid
alisema, kamti hiyo inayojumuisha viongozi wa dini, Vijana na wanawake inalengo
la kuhubiri amani pamoja na kushajihisha maadili
ambayo yatawafanya vijana kuishi katika ustaarabu wa jamii zao.
Kamati za dini mbali mbali imekua ikifanya kazi ya kutoa elimu ya utunzaji wa
amani kwa kushirikiana na shirika la
Norway Church Aid (NCA) kupitia mradi wake wa Swahili Coast kwa mashirikiano ya
ubalozi wa Norway nchini Tanzania.
Comments
Post a Comment