UISLAMU NA UMILIKI WA ARDHI KWA MWANAMKE
Je, ni vipi uislamu unampa nafasi mwanamke kumiliki
ardhi?
NA
FATMA HAMAD, PEMBA
Kwa
muda mrefu, kumekuwepo na dhana potofu katika
baadhi
ya jamii, hususan Zanzibar, kwamba mwanamke
hana
haki ya kumiliki ardhi.
Dhana
hii imejikita zaidi katika mila na tamaduni kuliko katika misingi ya dini ya Kiislamu.
Viongozi
wa dini na wanaharakati wa haki za
wanawake
wamekuwa mstari wa mbele kupinga
mtazamo
huo, wakisisitiza kuwa Uislamu unamtambua
mwanamke
kama mmiliki halali wa mali, ikiwemo
ardhi.
Ingawa
viongozi wa dini ya kiislamu wanapinga
mtazamo
huo, wanaeleza kuwa mwanamke ana haki ya
kurithi,
kununua, na kutumia mali au ardhi kwa ridhaa
yake
mwenyewe.
Kiongozi wa dini ya kiislamu kutoka kijiji cha Wingwi
Njuguni kisiwani Pemba Juma Othman Nahoda anasema ‘’Urithi ni haki ya mwanamke, na si hisani’’
Anasema katika Suratul- Nisa, aya ya saba (7) ‘’wanaume
wanafungu katika walichoachiwa na wazazi wao na
wanawake pia wanafungu katika walichoachiwa, iwe
kidogo au kikubwa, ni fungu lililowekwa’’.
Hii inamaanisha kuwa urithi wa ardhi au mali ni haki
ya mwanamke kwa amri ya Allah, na si kwa hiari ya
binadamu.
Sheikh Abdallah Mnubi Abass kutoka Jumuia ya Maimamu
Zanzibar
alinukuu Hotuba ya Mtume Muhammad
(S,A,W) :
‘’Mtume alisema Mali zenu, damu zenu, na heshima zenu
ni takatifu’’ hii inajumuisha mali ya mwanamke, ardhi
yake haichukuliwi kwa nguvu wala hila, bali kwa ridhaa
yake tu.’’
Sheikh Said Ahmed Mohamed kutoka Ofisi ya Mufti kisiwani
Pemba, anasema wanawake pia wanahaki ya kuchuma
na kumiliki.
Anasema katika aya ya 32 ya suratul Nisai, inaeleza
kuwa ‘’Wanaume watapata walichokichuma na
wanawake watapata walichokichuma.’’
Aya hii inathibitisha kuwa mali anayopata mwanamke
ni yake halali, akinunua ardhi, hakuna kizuwizi cha dini
kinachomzuia.’’
Hata Bi Amirat kutoka Jumuiya ya wanawake wa kiislamu
Pemba (JUMA WA KIPE) Asya Amour Abrahman anasema
Uislamu umemnyanyua mwanamke, hivyo kwa mujibu wa
Sheria ya Dini ya Uislamu na yeye anahaki ya kumiliki Ardhi.
‘’Mwanamke anahaki ya kumiliki ardhi na akaweza
kuitumia kwa shughuli za kilimo, na akajipatia kipato
kutokana na Shamba lake, isipokua kuna mipaka yake katika
suala la mirathi tu,’’anafafanua.
Anasema mwanamke anahaki ya kufanya shughuli zozote za
kimaendeleo na kujipatia kipato, ambacho kinakubalika
katika uislamu.
JAMII/WANAWAKE
WENYEWE
Fatma Mkubwa Ali mkaazi wa Mjini Ole ambae
anajishughulisha na kilimo Msitu anasema yeye ana miliki
shamba lake mwenyewe.
‘’Wazazi wangu walipofariki nilipewa ardhi yangu , na sasa
naitumia kwa shughuli za kilimo Msitu, nazalisha mazao,
kwa ajili ya chakula nyumbani na mengine ninakuja kuuza
nipate pesa,’’anasema.
Anasema umuhimu mkubwa wa mwanamke akiwa na ardhi
yake mwenyewe ni kujipatia kipato kwani anaweza kulima
kilimo cha muda mfupi na cha muda mrefu ambacho atapata
Chakula, Pesa pamoja na kulinda athari za mazingira.
Afisa sheria kutoka Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana Pemba, Massoud Ali Massoud , akiwakumbusha wananchi, wa Micheweni kurithi mali za marehemu mapema, ili kuepusha migogoro inayozuilika, kwenye mkutano wa kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, uliofanyika Skuli ya Michweni.
WANAHARAKATI
Kaimu Mratibu wa Chama cha Wandishi wa Habari
Wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar, Ofisi ya Pemba Amina Ahmed
Mohamed anasema wanawake wanahaki ya kumiliki ardhizao wenyewe kama Dini na
Sheria zinavyoelekeza.
Anasema moja ya mkakati wanaoufanya ni kuihamasisha jamii
kuhakikisha wanawake nawao wanakua na ardhi zao wenyewe, ima kwa kununua ama kurithishwa
wakati wanapofariki wazazi wao.
‘’Kutokana na janga la Mabadiliko ya tabianchi
linalotukumba,ni vyema wanawake nawao wakawa na ardhi zao wenyewe, ili wajipatie
kipato chao kutokana na ardhi zao wenyewe,’’anasema.
Sada Juma Segeja mtetezi wa masuala ya wanawake kutoka
Jumuia ya Uhifadhi wa misitu kisiwani Pemba CFP, anasema
bado jamii imekua na mitazamo potofu kwamba mwanamke
hawezi kumiliki ardhi.
Anasema moja ya changamoto inayowakabili katika mradi
wao wa uhifadhi mazingira ni baadhi ya wanawake kukosa
rasilimali Ardhi, kwa ajili ya kufanyia shughuli hizo za
uhifadhi, jambo linapelekea kuanguka kiuchumi, na
kuathirika na mabadiliko ya tabianchi.
‘’Katika mradi wetu wa uhifadhi wa mazingira ambao
tunautekeleza katika Shehia za Chwale, Mchanga mdogo,
Kambini na Mjini kiuyu, tunapata changamoto kubwa ya
baadhi ya wanawake kukosa ardhi zao wenyewe,’’anasema.
Anasema licha kwamba wanawake wamekua wakirithi
ardhi baada ya wazazi wao wanapofariki, bado mali hizo
huhodhiwa na kaka ama ndugu zao wa kiume, na kupelekea
wao kukosa sehemu ya kufanyia shughuli ambazo zinaweza
zikazalisha kipato.
NINI KIFANYIKE
Kwa mujibu wa viongozi wa dini, hakuna aya wala hadithi
inayomnyima mwanamke haki ya kumiliki ardhi, kinyume
chake uislamu unampa ulinzi, heshima kamili katika mali
yake, isipokua ni mila na tamaduni za jamii, hivyo ipo haja
sasa kuondokana na mila hizo kuona mwanamke na yeye
anamiliki ardhi yake mwenyewe, aweze kuzalisha na kujipatia kipato.
MIKATABA
Kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu
cha 12 (a) kinaeleza kuwa watu wote ni sawa mbele ya
Sheria, na wanayohaki, bila ubaguzi wowote, kulindwa na
kupata haki sawa mbele ya Sheria.
Hata Sheria ya ardhi Zanzibar namba 12 ya mwaka 1992
inaeleza kuwa ardhi ya Zanzibar ni mali ya umma, hivyo kila mwananchi anahaki
ya kutumia ardhi.
Mkataba wa Umoja wa Mataifa CEDAW wa mwaka 1986, unapiga
marufuku ubaguzi wa kijinsia katika umeliki wa mali.
Itifaki ya Maputo (kifungu cha 21) inahakikisha wanawake
wanapata urithi bila kubaguliwa na tamaduni.
Makadirio ya Bajeti
kwa mwaka wa Fedha
2023/2024 ya Wizara ya Ardhi na
Maendeleo ya Makaazi,
Kuendelea kutoa elimu
kwa jamii kuepuka
kujiingiza kwenye migogoro
ya ardhi kwa kufuata
Sheria za ardhi
Katika tamko la Machi 2024, lilotolewa na Chama cha Wandishi
wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) Zanziba
linasisitiza kwamba ‘’Sera za jinsia lazima ziwepo katika sekta zote,
ili wanawake wasiachwe nyuma.’’
Kwa mujibu wa Utafiti alioufanywa na Mkurugenzi wa Chama
hicho Mzuri Issa Ali, mwaka 2025, ulionesha kuwa mitazamo ya jamii na vyombo
vya habari vina nafasi kubwa katika kuendeleza au kupunguza mitazamo hiyo
potofu.
MITANDAO
YA KIJAMII/MWANANCHI
Mkurugenzi wa huduma za kisheria wa kituo cha sharia cha
Haki za binadamu(LHRC), Funlgence Massawe anasema serikali imepiga hatua kubwa
katika kurekebisha sharia zinazokua zinakwamisha umiliki wa ardhi kwa wanawake.
Mkurugenzi huyo ameyasema hao Novemba 26, 2020 jijini Dar es
Salaam wakati akichangia kwenye mjadala wa Jukwaa la Fikra lililoandaliwa na
kampuni ya Mwananchi Communication ltd (MCL), anasema tofauti ya kipato ni
sehemu kubwa inayochangia ukatili wa kijinsia, huku akigusia katiba ya Tanzania
kuhusu haki ya kila mtu kumiliki mali, akisisitiza kuwa haijasema mwanamme au
mwanamke bali mtu yoyote.
Anasema sheria ya
mirathi inamatatizo na inatakiwa kufanyiwa marekebisho ili kutoa fursa kwa
wanawake tofauti na ilivyo sasa.
Anabainisha kuwa ardhi ndio chanzo kikubwa cha migogoro
katika jamii na wanawake wamekua wakinyanyaswa kwa kunyimwa umiliki wa ardhi.
Comments
Post a Comment