Watendaji wa wizara ya maji kisiwani, Pemba wamelalamikia kunyimwa haki zao

 


Watendaji wa wizara ya maji kisiwani, Pemba wamelalamikia juu ya ukosefu  wa haki na fursa za kielimu ambazo zimekua zikipatikana kupitia wizara hio kwa muda mrefu sasa.

Malalamiko hayo wameyatoa mbele ya waziri wa wizara ya maji na nishati Zanzibar Sleimani Masoud Makame,wakati alipokutana na watendaji wa wizara hio kisiwani Pemba ambapo watendaji hao  wamedai kua wamekua wakikoseshwa fursa mbalimbali kutoka wizara hiyo ikiwemo fursa ya mafumzo.

‘’Mheshimiwa Waziri Mkurugenzi wetu mtu aliekua hana elimu ndio anaempa kipao mbele na maranyingi huwateuwa nafasi kubwa wale waliokua hawana elimu’’Walisema  wafanyakazi wa wizara hiyo.




Baada ya kupokea malalamiko hayo waziri wa wizara hio amemuagiza mkurugenzi  wa mamlaka ya maji Pemba Omari Mshindo Bakari, kushughulikia upatikanaji wa stahiki za wafanyakazi hao.

‘’Mkurugenzi naomba kuanzia sasa kila mmoja hakikisha anapata haki yake, sitaki kuletewa  tena malalamiko ya mtu kakosa haki yake’’Alisema Waziri.

Aidha waziri huyo amewataka wafanya kazi wa Mamlaka ya Maji kutekeleza majukumu yao  ipasavyo bila ya ubaguzi, huku akiahidi kusimamia vyema haki za wafanya kazi hao .

‘’Acheni ubaguzi, acheni kufarakana, acheni kugawana  naombeni mfanye kazi kwa mashirikiano’’Alisema waziri wa Suleiman.

Mbali na agizo hilo la kutaka kulipwa stahiki za wafanya kazi hao,  waziri amesema wizara yake hatomvumilia mtendaji wa wizara hiyo atakaebainika anafanya ubadhirifu wa mali  nakuahidi kuashughulikia watakao shindwa kuajibika kazini.


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.