JAMII YAHIMIZWA KUTUNZA USAFFI MAZINGIRA

 

NA SAID ABRAHMAN PEMBA.

 WANAJAMII wametakiwa kutunza mazingira yao na kuhifadhi maji taka ( maji machafu) ili kuepusha maradhi ya mripuko yanayoweza kutokezea katika maeneo yao.

 Hayo yalielezwa na Bwana afya kutoka Baraza la Mji Wete Salim Mbarouk Rashid wakati alipokuwa akizungumza na Mwandishi wa habari hizi huko Ofisini kwake Wete.

 Alieleza kuwa kumekuwepo na utiririkaji Mkubwa wa maji taka (machafu) katika majumba jambo ambalo ni tatizo kubwa Kimazingira na hivyo kufanya mazingira kuwa katika hatari na kuwa Kero katika jamii.

 "Kutokana na Hali ambayo ipo katika jamii,suala la kutiririka Kwa maji taka linahatarisha afya Kwa wananchi na hivyo kupelekea kuibuka Kwa maradhi mbali mbali ya miripuko ikiwemo matumbo na kipindupindu," alieleza Salum.

 Aidha Salim alifahamisha kuwa ikiwa Baraza la Mji Wete ndio wasimamizi wakuu wa Usafi katika Mji wamekuwa na mikakati mbali mbali ili kuona hali hiyo inapungua au kuondoka kabisa katika jamii.

 "Mikakati ambayo tumejipangia sisi Baraza la Mji Wete kuondosha hii kadhia ya kutiririka Kwa maji taka kwanza ni kufanya ukaguzi wa mara Kwa mara katika majumba ili kuweza kuwapa elimu Wana jamii jinsi ya kudhibiti maji hayo (maji machafu) kwani imeonekana maji taka imekuwa ni tatizo kubwa katika jamii na Kwa Serikali Kwa ujumla," alisema Afisa Salim.

 Mbali na hayo lakini pia Baraza limekuwa likihakikisha kuwa maji taka (maji machafu) yanadhibitiwa Kwa kuwapatia elimu Wana jamii juu ya afya pamoja na kutunza mazingira.

 "Sababu kubwa ambayo inaonekana kutiririka Kwa maji taka (machafu) ni pale wanajamii wanapoamua kujenga nyumba zao Huwa wanasahau kuchimba shimo la kuhifadhia maji hayo na badalayake wao wanachimba shimo moja tu la kinyesi ilhali kunahitajika mashimo mawili, kwani sheria ya mazingira ya mwaka 2011 na 2012 Namba 11 imeelekeza hivyo," alisema Salim.

 Sambamba na hayo Afisa huyo alieleza kuwa wamegunduwa Kwa wanajamii wengi hawaelewi umuhimu wa utumiaji wa shimo la utumiaji wa maji taka na ndio maana Baraza likaweza kuchukuwa dhima la kutoa taaluma Kwa wananchi wote.

 Akizungumzia suala la adhabu Kwa mwananchi ambae atapatikana na hatia ya kutiririsha maji machafu katika nyumba yake, afisa huyo alisema kuwa Kwa upande wa Baraza ni faini ya Tsh, 20000/- ambapo faini hiyo ni ya papo Kwa papo huku akitakiwa kuchimba shimo Hilo mara moja.

 "Kwa upande wa adhabu, mwananchi ambae atapatikana na kosa hili ni faini ya Tsh, 20,000/ ya papo Kwa papo na baadae kuchimba shimo na endapo hakufanya hivyo tunampeleka Mahakamani na adhabu yake ni kifungo kisichopungua miezi (6) na faini laki 3 (300,000/-) alisema Salim.

 Mapema afisa huyo alifahamisha kuwa kazi za kitengo Cha afya Baraza la Mji ni kuhakikisha kinasimamia Usafi wa mazingira, kusimamia uondoshaji wa taka ngumu ambazo zinazalishwa katika maeneo mbali mbali ya Mji wa Wete.

 "Lakini pia kitengo hichi kina dhima ya  kusimamia suala la Usafi barabarani pamoja na kuhakikisha mitaro yote iko katika hali ya Usafi," alieleza Salum.

 

            

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.