WASTAAFU WATARAJIWA WAFUNDWA

 

                      NA FATMA HAMAD FAKI PEMBA.

Kaimu mkurugenzi wa huduma kwa wateja kutoka  mfuko wa hifadhi ya jamii ZSSF Khatib Iddi Khatib amewataka wafanyakazi katika tasisi za umma kuwa na utaratibu wa kuamzisha miradi nbali mbali wanapokuwa kazini ili iwasaidie  mara watakapo staafu.

Ushauri huo ameutoa wakati akiwasilisha mada juu ya matayarisho ya kustaafu katika mkutano wa mafunzo ya  wastau watarajiwa uliofanyika katika ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake chake Pemba.

Amesema Kila mtumishi wa umma kwa vile ameajiriwa ajuwe kama kuna siku ataondoka, hivyo ni vyema kubuni mbinu mbadala ikiwemo kuweka miradi  ambayo itawapatia kipato cha halali katika maisha yao ya kustaafu kwao.

‘’hatuwezi kudumu milele makazini tukubali kuwa ipo siku tutaondoka hivyo ni lazima  tuweke vyanzo ambavyo vitakuja kutupatia kipato Pencheni sio kama mshahara haitoshi kuendesha maisha yetu’’alikumbusha kaimu mkurugenzi.

Akifungua mafunzo hayo Ofisa mdhamini wizara ya Nchi Fedha na Mipango Abdul wahab Said Abubakar amewataka watarajiwa hao kuwahimiza wafanya kazi wenzao kufanya kazi kwa uadilifu na kwa uwangalifu ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi jambo ambalo litawafanya waweze kupata haki zao stahiki kutoka Zssf.

Mapema akitoa mada juu ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza Dk Rahila Salim  Omar amesema watu wengi wanaposatafu hupata maradhi mbali mbali ikiwemo  kupooza hivyo ni vyema Zssf kuwa na muendelezo wa kutoa mafunzo kwa watarajiwa wastafu ili waweze kuondokana na hofu jambo ambalo litaepusha kupata shida kama hizo.

 Baadhi ya watarajiwa hao wastaafu wameishari Ofisi ya Zssf kuweka vituo vya Hospitali maalumu ambavyo vitatoa huduma kwa wafanya kazi watakao staafu.

Nae mkuu wa kitengo cha uhusiano na elimu Zssf Raya Hamdan Khamis amesema lengo la mafunzo hayo kwa wastaafu watarajiwa ni kuwakumbusha juu ya kujitayarisha  na wakati wao wa kustafu ili waweze kukabiliana na hilo








Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.