KIRARE AFUNGWA JELA

 

NA FATMA HAMAD PEMBA

Mahakama ya mkoa C iliyopo Chake chake imemuhukumu kijana Khamis Abdala Khamis maarufu  [Kirare]  mwenye umri wa miaka 20 mkaazi wa Kangani  wilaya ya Mkoani Pemba kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 19 na fidia ya shilingi Milioni mbili[200,000] baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kutorosha na kulawiti mvulana wa miaka 10.

Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka [DPP] Ali Amour Makame ameiambia mahakama hiyo kuwa mtuhumiwa huyo makosa yote mawili alioyafanya ni makubwa na kwa maelezo kutoka kwa daktari ni kwamba amesababisha ulemavu kwa mhanga, hivyo naiomba mahakama yako itowe adhabu kali ambayo itakuwa ni funzo kwake na wengine wanaotenda makosa hayo.

‘’Jamii imekua ikisikitika sana kwa matendo haya ya kihalifu hivyo nivyema mahakama yako ikampa adhabu kali kijana huyo’’ alidai Dpp Ali.

Hakimu wa mahakama hiyo Muumin Ali Juma amemueleza  mtuhumiwa kwamba mahakama imekuona na hatia kwa makosa yote mawili la kutorosha na kulawiti,hivyo kwa mujibu wa kifungu cha 299 sheria nambari 7/2018 sheria ya Zanzibar kosa la kwanza utatumikia chuo na Mafunzo kwa muda wa miaka 5, ambapo kosa la pili la kulawiti kwa mujibu wa kifungu cha 7[a] sheria namba 7/2018 sheria ya Zanzibar utatumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 14.

 

 Kabla, ya hukumu huyo, mshtakiwa Khamis Abdalla Khamis ‘kirere’ miaka 20 wa Kangani wilaya ya Mkoani Pemba, alimtorosha na kisha kumlawiti mtoto wa miaka 10.

Ambapo alimtorosha kutoka sokoni Kangani na kumpeleka kwenye banda analolala, ambaapo hilo ni kosa kinyume na kifungu cha 113 (1) (b) cha sheria ya Adhabu sheria namba 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

Huku kosa la pili alilotiwa hatiani ni la utawiti, wa mtoto huyo ambalo ni kosa kinyume na kifungu cha 115 (1) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

                                   

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.