JAMII YAHIMIZWA KUONGEZA USHIRIKIANO ILI KUMALIZA UDHALILISHAJI UDHALILISHAJI

 







                

               NA FATMA HAMAD FAKI PEMBA 23/11/2022.

Jamii imetakiwa kuacha tabia  ya kuzifanyia suluhu  mitaani kesi  za udhalilishaji wa kijinsia  na badalayake  wasimame mahakamani  kutoa ushahidi ili kupunguza ukatili  kwa wanawake na watoto.

Ushauri huo ametolewa na mwenyekiti wa kamati za asasi za kiraia Nassor Bilal Khamis wakati akitoa tarifa kwa vyombo vya habari katika  kuelekea  shamra shamra ya madhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili kwa wanawake na watoto huko tamwa chake chake Pemba.

Amesema  bado matendo ya udhalilishaji yafanyika kila siku katika shehia zetu, hivyo ni wakati jamii kuondosha rushwa muhali ili kuona wahanga wa matukio hayo wanapata haki zao stahiki.

‘’kwa kweli jamii imekua na muhali mkubwa juu ya kusimama mahakamani na kutoa ushahidi kwenye vyombo vya kisheria matukio ya udhalilishaji’’ alisema mwenyekiti.

Amesema kwa mujibu wa ripoti za takwimu za ukatili na udhalilishaji wa kijinsia  Zanzibar takwimu kutoka ofisi ya mtakwimu mkuu wa Serikali jumla  matukio 131 ya ukatili na udhalilishaji yameripotiwa katika kipindi cha mwezi Agosti 2022  mwaka huu ambapo wanawake ni 12, Watoto 119 miongoni mwao wasichana ni  84 na wavulana  35.

Kwa upande wake mratibu wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Zanziba [Tamwa] ofisi ya Pemba Fathiya Mussa Said amewasihi wanasheria  wanaosimamia  kesi mahakamani kufuata madili na miko ya kazi zao.

‘’Niwaombe mawakili  msimamie kesi kwa mujibu wa madili yanu kwani leo kafanyiwa mtoto wa mwenzako kesho atafanyiwa wa kwako’’ alisema mratibu tamwa.

Madhimisho ya 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji yatanza rasmi tarehe 25 mwezi huu ambapo kutakua na shughuli mbali mbali ikiwemo utolewaji wa elimu ya udhalilishaji na jinsi ya kuripoti katika vyombo vya sheria kupitia shehia na kwenye madrasa kwa wilaya zote za pemba.

 

 

 


   

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.