Waandishi wa Habari Pemba Watakiwa kutoa elimu kwa vyama vya siasa juu ya nafasi ya mwanamke.


 



Wandishi wa habari wametakiwa kutoa elimu kwa vyama vya siasa waweze kutoa fursa sawa za uongozi kwa Wanawake na Wanaume ili kuona Wanawake na wao wanashika nafasi za uongozi katika ngazi mbali mbali za maamuzi.

Hayo yamesemwa na mwezeshaji wa mafunzo ya uhamasishaji wa Wanawake katika ushiriki wa Demokrasia na uongozi kwa wandishi wa habari huko Ofisi za Tamwa Mkanjuni Chake chake Pemba.

Amesema imeonekana bado hakuna uwiano sawa baina ya wanaume na Wanawake katika ngazi mbalimbali za maamuzi, hivyo ni jukumu la wandishi wa habari kuwa eilimisha viongozi wa vyama vya siasa kuondosha vikwazo ambavyo vinawakosesha fursa ya uongozi wanawake wenye nia ya kugombea.

‘’Ni jukumu lenu Wanahabari kuwapa elimu viongozi wa kisiasa kuondosha vikwazo vinavyowafanya wanawake washindwe kuwa viongozi’’. Alisema Bi sabah.

Amesema mwanamke ana nafasi kubwa ya kuwasilisha matatizo ya jamii yakiwemo ya Wanawake katika vyombo vya mamuzi kwa kulinganisha naWanaume.

Hivyo ameisihi jamii kuondosha dhana potofu na badala yake waone kwamba mwanamke na yeye anaweza kuwa kiongozi.

Hadia Faki Juma mshiriki wa mafunzo hayo amesema mfumo dume uliopo kwa vyama vya siasa pamoja na jamii umekuwa ukiwakatisha tama wanawake walio na nia ya kugombea.

Nae Suleiman Rashid Omar ambae pia ni mshiriki wamafunzo hayo amesema ni vyema Wanawake kulipa kipao mbele suala la Elimu jambo ambalo litawajengea uwezo wanawake wakati watakapopata fursa za uongozi.

Mafunzo hayo ya siku nane kwa wandishi wa habari yameandaliwa na chama cha wandishi wa habari wanawake Zanzibar Tamwa,  Zafela pamoja na Pegao kwa kushirikiana na Ubalozi wa Norway Nchini.

 




Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.