VIONGOZI WA DINI WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA JAMII JUU YA UMUHIMU YA MWANAMKE KUWA KIONGOZI


 

Viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kuielimisha jamii juu ya  umuhimu wa mwanamke kushika nafasi za ungozi katika ngazi mbali mbali za kutunga Sheria.

Akizungumza na viongozi wa dini ya kiislamu Kisiwani Pemba  Afisa fatwa kutoka ofisi ya Mufti Sheikh Said Ahmad Muhammed katika mkutano wa uwasilishwaji wa ripoti ya miezi mitatu juu ya mwanamke kuwa kiongozi huko  Tamwa  Chake chake Pemba.

Sheikh Said alisema Uislamu hauja mkataza mwanamke kua kiongozi ilihali tu afuate Sheria,Mila na Maadili yake .

‘’Dini haijamzuia mwanamke kuwa kiongozi bali afuate sheria na Madili ya dini yake’’ Alisema Sheikh Said.

Hivyo alisema wakati umefika kwa viongozi wa dini mbali mbali kutoa elimu kwa jamii ili kuhakikisha mwanamke nayeye anashiriki katika nafasi mbali mbali za uongozi.

Aidha Shikh Said amewataka wazazi na Walezi kutowabagua watoto  Kijinsia  katika kutoa fursa za kuwapatia Elimu.

Wakichangia katika mkutano huo baadhi ya viongozi hao  walisema kuwa ipo haja ya kutolewa elimu kwa Masheikh na maimu pamoja na wanajamii  ili kufahamu kwamba mwanamke nayeye anaweza kuongoza.



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.