UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.
NA FATMA HAMAD, PEMBA …………….. SIRI ya mtungi aijuaye kata……… Wahenga wametupa usia usemao ……Hasira hasara. Wakati mwengine hio hasira sio tu huathiri aliyefanya na aliyefanyiwa, bali watu wa karibu, mbali na hata jamii kwa ujumla. Hili linaonekana sana pale ndoa inapovunjika baada ya wana ndoa kuamua lipasuke tugawane mbao, lakini misumari ya hizo mbao huwachoma na kuwaumiza wengi, wakiwemo wana familia na hasa watoto. Mara nyingi pale wazazi wakiwa wametengana baada ya ndoa kuvunjika watoto hukosa huduma muhimu za maisha na kuathirika kimwili na kiakili na kiza hutanda katika safari yao ya maisha. Mwana harakati maarufu wa kulinda na kutetea haki za watoto kisiwani Pemba, Tatu Abdala Mselem, amekuwa mara kwa mara akiiomba jamii kuvunjika kwa ndoa isiwe sababu ya kila mzazi kufumbia macho wajibu wake wa malezi ya watoto. Hii ni kwa sababu mtoto anapokosa huduma za lazima sio tu huwa mnyonge na kujiona kama yatima aliyekosa msaada, bali huwa hana furaha anapocheza, na akili yak
Comments
Post a Comment