KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME
NA FATMA HAMAD- PEMBA WANANCHI WA KIJIJI cha Gombeume Shehia ya Mchangamdogo Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba, wamelalamikia juu ya ukosefu wa huduma ya Maji safi na salama kijijini hapo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwao Gombeume mwananchi Bishamba Suleiman Ali na Fatma Said Haji wamesema huu ni zaidi ya mwaka wa tatu hawapati huduma ya maji katika kijiji chao. Walisema wamechoka na kadhiya hiyo ambayo inawafanya waende mabondeni kufuata huduma ya maji, kwa ajili ya matumizi ya majumbani mwao. ‘’Kwakweli tuna shida kubwa wananchi wa gombeume, tunakwenda mabondeni kwenye visima vya zamani kuchota maji, tunaumia na tumechoshwa na shida hiyo,’’walisema. Walisema wanahofu ya kujakupata m...
Comments
Post a Comment