NUHU KOMBO NUHU AENDELEA KUSOTA RUMANDE


 NA FATMA HAMAD-- PEMBA.

Hatimae mahakama ya mkoa B Wete, imemrejesha tena rumande mtuhumiwa wa ulawiti Kombo Nuhu Kombo miaka 19 baada ya kubainika kuwa ni mtu mzima licha ya awali kupewa dhamana kama ni mtoto mahakamani hapo.

Awali mtuhumiwa alipelekwa rumande mwanzoni mwa mwaka huu kwa tuhuma za ulawiti kwa kijana mwenye ulemavu wa akili ingawa upande wa utetezi ulidai na kuthibitisha kuwa mteja wao hakutendewa haki kupelekwa rumande kwa sababu ni mtoto.

Wakati kesi yake ikiendelea miezi mitatu iliyopita  na kuwasilishwa  vielelezo mahakamani hapo na upande wa utetezi mahakamani  iliridhia na kumpa dhamana mtuhumiwa huyo  kama mtoto.

Huku upande wa mashtaka ukiendelea kung’ang’ania  kwamba mtuhumiwa ni mtu mzima, kisha uliwasilisha vielelezo kadhaa ikiwemo cheti cha kuzaliwa cha mtuhumiwa na mahakama kutengua uwamuzi wake wa awali juu ya umri wa mtuhumiwa.

Mwendewsha mashtaka katika shauri hilo Juma Ali Juma alidai mahakamani hapo kuwa anaelewa kuwa mtuhumiwa Nuhu Kombo Nuhu  ni mtu mzima na hakupaswa kupewa dhamana kwa kisingizio cha kuwa ni mtoto.

Ndipo April 13 mwaka huu kesi hiyo ilisomwa tena upya mbele ya hakimu Ali Abdulrahman Ali na kuamuru mtuhumiwa huyo kurejeshwa tena rumande baada ya vielelezo vyake vilivyokubaliwa  na kuonyesha kwamba ni mtu mzima.

“ April 5 mwaka huu baada ya kupokea vilelezo na kujiridhisha juu ya umri wa mtuhumiwa dhamana yake imefutwa na sasa atarudi tena rumande na kurejea tena mahakamani hapa April 27 mwaka huu kuendelea na kesi yake” , alisema.

Awali mtuhumiwa huyo alipandishwa mahakamani hapo akikabiliwa na tuhuma za kumlawiti kijana mwenye ulemavu wa akili mwenye miaka 19 jambo ambalo ni kosa kisheria

Tukio hilo lilitokea tarehe 13/ 12/ 2021 majira ya sa moja asubuhi huko kijichame wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba ambapo mtuhumiwa alimlawiti kijana mwenye ulemavu wa akili.

Ilidaiwa kuwa kufanya hyivyo ni kinyume na kifungu cha 116[1] cha sheria nambari 6/2018 sheria  ya Zanzibar.

                       

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.