UDHALILISHAJI BADO NI KILIO KWA WANAWAKE NA WATOTO
NA FATMA HAMAD- PEMBA.
Mahakama maalum
inayoshughulikia kesi za udhalilishaji mkoa wa Kusini Pemba imeihairisha kesi
ya ubakaji inayomkabili mtuhumiwa Ali Usi Simai mtumzima wa miaka 32 mkaazi wa Mchakwe
Muambe anaedaiwa kumbaka msichana wa
miaka nane (8)ambapo kufanya
hivyo ni kosa kisheria.
Akizungumza mbele ya Mahakama hiyo mwendesha mashtaka wa
Serikali kutoka Ofisi ya mkurugenzi wa
mashtaka DPP Seif Mohd Khamis ,aliiambia
mahakama iihairishe kesi hiyo kwani
upande wa mashtaka hawakupokea
chaji shiti ya kesi wenyewe.
“Mheshimiwa sikupokea chaji shiti, kwa hivyo siwezi
kucheza na haki ya mtu kwani sijui
kilichoandikwa kwenye file hilo naomba uipangie siku nyengine ili niweze
kulipitia’’, alisema DPP Seif.
Kwa upande wake wakili wa kujitegemea Saleh Said Moh’d
alisema hakubaliani na ombi hilo kwani
wamekuja na mashahidi 4 akiwemo
mwenyewe mtuhumiwa, hivyo kuihairisha
itakuwa shida lazima tuwaangalie
mashahidi wenyewe wametoka mbali jambo ambalo kuja na kurudi itawaumiza.
Hakimu wa mahakama hiyo Muumin Ali Juma alisema
amekubaliana na upande wa mwendesha mashtaka wa
Serikali kwamba hawezi kufanya utetezi kwani hajui kilichoandikwa kwenye
file hilo, hivyo hatutoisikiliza kesi hiyo na itarudi tena tarehe 19/3 mwaka huu kwa ajili ya kusikilizwa.
Mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo ambapo ni kosa kinyume
na kifungu cha 108 (1) (2) (e) na 109 (1) sheria nambari 6 ya mwaka 2018 sheria
ya Zanzibaer.
Comments
Post a Comment