KUKOSEKANA MKALIMANI MASKULINI BADO NI TATIZO KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU

 

NA FATMA HAMAD-- PEMBA.

Kukosekana kwa walimu wanaojua lugha za alama maskulini bado ni kilio kikubwa kinacho wa kwaza wanafunzi wenye ulemavu kisiwani Pemba.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwao Kwale gongo wilaya ya Wete kaskazini Pemba, wazazi wa watoto wenye ulemavu walisema suala la kuchanganywa darasa  pamoja na wanafunzi wengine bila ya kuepo kwa  mwalimu wa lugha za alama kunachangia wanafunzi hao kutofaulu mitihani yao na kusababisha kushindwa kufikia malengo yao.

‘’Mfumo wa elimu mjumuishi wa kuchanganywa pamoja na wanafunzi wenye ulemavu na  wengine  bado hauja watendea haki watu wa aina hiyo  maskulini,’’ alisema mama mzazi wa Abdala Hussein mwenye ulemavu wa uziwi, mdomo na mguu.

Alisema mtoto wake anasoma darasa la kumi ila hana tamaa ya kufaulu kutokana na changamoto hiyo  na kuiomba  wizara ya elimu kumuona  kijana huyo na kuweza kumsaidia kwa hali na mali ili kuona na yeye amekuja na ufaulu mzuri.

Akiendelea kueleza kwa masikitiko mama huyo alisema kiukweli wanafunzi wenye ulemavu  kitendo cha kwenda Skuli ni kwenda kupoteza muda tu ila lengo hasa la kusomana kufaulu  halipo.

Kwa upande wake baba mzazi wa Salum  Said Asaa mwenye ulemavu wa macho  alisema  kuwa yeye mtoto wake alishindwa kumpeleka skuli kwani anahisi ni kwenda kupoteza muda tu haoni anachokwenda kukisoma na kukifahamu.

‘’Mimi mtoto wangu angalikuwa  alishafika darasa la pili ila nimeshindwa kumpeleka skuli kwani hakuna mwalimu wa kumfundisha yeye , bali  namuacha ande chekechea tu ili apoteze muda tu”, alieleza mama mzazi wa Salum.

Mzazi huyo aliitaka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kufanya jitihada ya kujenga skuli maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu ili kuona na wao wanasoma na kupata ajira.

Nae mwalimu mkuu wa Skuli ya Kinyasini iliyopo Wete Pemba Asha Mbarouk Rashid alisema kwa kweli wanapata shida kufundisha wanafunzi wenye ulemavu kwani hawana taaluma hiyo na wala hawana mwalimu hata mmoja anejua lugha ya alama.

‘’Kwa kweli wanafunzi wenye ulemavu huwa hatuwarejeshi tuna wapeleka  mbele tu  alimradi wamalize masomo yao wapumzike, ila hawana wanacho kisoma na wala hawawezi kufaulu mitihani yao”, alieleza mwalimu mkuu.

Alisema kwa kweli matokeo ya wanafunzi wenye ulemavu ni mabaya, hivyo jitihada za makusudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zinahitajika ili kuona inasomesha walimu wengi wa elimu mjumuishi.

Hata hivyo alieleza kuwepo  kwa  mwalimu wa aina hiyo kunaweza kuwafanya wanafunzi hao kupata vyema haki zao za msingi ya elimu  na kuhakikisha wanafaulu mitihani yao na kufikia upeo wa akili zao.




                     

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.