KAMATI ZA ULINZI NA USALAMA PEMBA ZA TAKIWA KUWA WADILIFU WAKATI WA UKODISHWAJI WA MASHAMBA YA MIKARAFUU



NA LAILAT MSABAH PEMBA.

Kamati za ulinzi na usalama katika mikoa miwili ya Pemba zimetakiwa kuwa makini katika kusimamia zoezi la ukodishwaji wa mashamba ya karafuu ya Serikali ili kuona misingi ya ukodishaji wa mashamba hayo inafuatwa na kuepusha upotevu wa mapato ya serikali.

Akizungumza katika kikao na kamati iliyoonda kusimamia ha ukodishwaji wa mashamba hayo Mkuu wa Mkoa wa kaskazi Pemba Salama Mbarouk Khatibu amesema kamati hizo zinao wajibu mkubwa wa kuona mashamba ya karafuu yanakodishwa katika hali ya amani bila ya kuwepo na migogoro.

‘’Munadhamana kubwa kuhakikisha hakutokei migogoro yoyote wakati wa zoezi hilo la ukodishwaji mikarafuu’’ Alisema bi salama.

Amewafahamisha kuwa endapo watasimamia zoezi hilo kwa uadilifu wa hali ya juu  na kufuata taratibu zilizowekwa kutasaidia kuiongezea Serikali mapato yanayotokana na zao la karafuu.



 Mkuu wa wilaya ya Wete Mgeni Khatibu Yahya ameziomba kamati za ulinzi na usalama kufuatilia maeneo ambayo tayari uchumaji wa karafuu umeanza na kuhoji wapi zimechumwa .

‘’Nivyema  mukapita panapoanikwa mukahoji, isjekua wanachuma katika yale mashamba ya Serikali yatakayo kodishwa’’ Alisema mkuu wa Wilaya

 Wete 

Mapema Afisa Mdhamini wizara ya kilimo, Umwagiliaji, Mali Asili na Mifugo Hakim Vuai Shein ameitaka kamati itakayo simamia zoezi la ukodishaji wa mashamba  kufanya kazi kwa mashirikiano na wizara hiyo ili kuepusha malalamiko yanayojitokeza kama ilivyokua  misimu uliyopita .

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo imekuwa na utaratibu wa kukodisha mashamba ya karafuu kwa kila inapofika msimu na wakati mwengine kumekuwa kukiibuka malalamiko ya wananchi na wakulima juu ya kutofuatwa kwa utaratibu wakati wa ukodishaji wa mashamba hao.









Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.