NA FATMA HAMAD PEMBA
Jamii imeonywa kuacha tabia yakuwaficha
wahalifu wanaowafanya matukio ya udhalilishaji wa kijinsia na kuzifanyia suluhu
kesi za hizo majumbani jambo ambolo linapelekea kuongezeka kwa vitendo vya
udhalilishaji.
Akizungumza na Wazazi na Walezi
katika mkutano wa kuielimisha jamii juu ya athari za udhalilishaji katibu wa
kamamati ya madili Zanzibar Abdala Mnubi Abass huko Tumbe wilaya ya Micheweni
Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Amesema vitendo vya udhalilishaji
vinajitokeza siku hadi siku, lakini bado jamii inaonekana ikizifumbia macho
na kuzifanyia suluhu kesi hizo wenyewe
kwa wenyewe.
‘’ wakishafanya makosa ya
udhalilishaji mna watorosha watoto wenu, wazazi wacheni hii tabia, Alisema
Abdala Mnubi’’.
Amesema wengi wafanyaji wa matukio
hayo ni watu wa karibu katika familia, hivyo wazazi wanapodhalilishiwa watoto
wao wasiwaonee haya wala wasiogope maneno ya mitaani bali wasimame kidete na kuwaripoti katika vyombo vya sheria ili
kuchukuliwa hatua kali dhidi yao.
Hata hivyo Mnubi amewaasa watoto
wasikubali kupokea zawadi au kitu chochote watakachopewa na watu njiani jambo
ambalo litawaepusha na udhalilishaji.
Baadhi ya wazazi walioshiriki mkutano
huo wamesema nivyema Jamii kushirikiana katika malezi ya pamoja kama ilivyokua
zamani ili kupata kizazi chenye madili bora.
Comments
Post a Comment