WIZI WA MBUZI WAMSABABISHIA KWENDA JELA PEMBA


NA FATMA HAMAD PEMBA  11/6/2021.

Jeshi la Polisi  Mkoa wa Kusini Pemba limefanikiwa kuwakamata watu 30 wanaotuhumiwa kujihusisha  na matukio mbali mbali ikiwemo wizi wa mazao pamoja na  mifugo.

Akizungumza na Wandishi wa habari huko ofisini kwake Madungu  Kamanda wa polisi mkoa huo Richad Mchovu amesema watuhumiwa hao wamewakamata kupitia opereshen ya wiki moja iliofanywa na jeshi hilo   Mkoani hapa kwa ajili ya kupambana na uhalifu ambao wanafanyiwa wananchi katika Vijiji vyao.

Amesema wahalifu hao 30,  saba ni wezi wa mifugo,  sita ni wezi wa mazao katika maeneo tofauti ,  wawili ni wezi wa mbuzi, wanne  walikamatwa maeneo ya mtambile wakiwa wameiba ngombe 3, watatu walikamatwa na madawa ya kulevya  na  kumi na mbili ni   wizi wa kuku.

Amefahamisha kuwa  mmoja  wawili kati ya hao walioiba mbuzi tayari hatua za kisheria zimeanza kuchukuliwa dhidi yake na ameshahukumiwa  kutumikiwa chuo cha mafunzo.

Aidha amesema upareshen hiyo bado inaendelea hivyo amewataka wananchi wanasafirisha mazao yao kupeleka sokoni kuchukua vibali kwa sheha ili kuondokana na usumbufu bara barani jambo ambalo litasaidia kuwakamata kwa urahisi wahalifiu wanaojishuhulisha na vitendo hivyo.

Kamanda mchovu ameoa wito kwa Wananchi kushirikiana na jeshi hilo kuwafichua wahalifu na kuwapeleka vituoni ili sheria ichukue naeasi yake jambo ambalo litapelekea kuishi kwa amani mitaani mwao.

 



 

 

 

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.