Wawili washikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za wizi wa mifugo.





FATMA HAMAD FAKI -  PEMBA.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba linawashikilia vijana wawili wakituhumiwa kwa wizi wa mifugo huko Kiwani na Mgagadu Wilaya ya Mkoani  Mkoa wa kusini Pemba.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba ACP Richard Tadei Mchovu amewataja vijana hao kuwa ni Moh`d Salum (35) Mkaazi wa Kilimani Mgagadu na Yussuf Rashid Moh`d  (30) Mkaazi wa Nanguji Kiwani katika Wilaya ya Mkoani Pemba ambapo wamekamatwa afajiri ya jana June 21 wakiwa na ng`ombe kwenye gari aina ya keri..

Akizungumza na waandishi wa habari huko ofisini kwake Madungu Chake Chake Kamanda Mchomvu amesema watuhumiwa hao wamekatwa na ng`ombe na wawili katika operesheni iliyofanya na jeshi hilo la kudhibiti wizi wa mifugo.

Aidha Kamanda Mchovu ametoa wito kwa wananchi kushirikiana pamoja katika kuzuia wimbi la wizi wa mifugo ambalo limekithiri katika maeneo mbali mbali huku akitoa wito kwa wafuagaji kuwa makini katika uangalizi wa mifugo yao.

Kwa upande mwengine Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba ACP Mchovu amesema jeshi hilo pia limefanikiwa kukamata mifugo mengine mbali mbali ya wizi kwenye mkoa huo ikiwemo ya mbuzi na kuku.

Jumla ya kesi 10 za wizi wa mifugo zimeripotiwa tokea kuanzishwa kwa kampeni ya “Familia yangu haina Uhalifu” ilionzishwa na jeshi la Polisi Mkoa wa kusini Pemba katika kukabiliana vitendo vya uhalifu, ikiwemo, wizi, na udhalilishaji.

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.