`UCHELEWESHWAJI WA UENDESHWAJI WA KESI MAHAKAMA KUNASABABISA MASHAHIDI KUSHINDWA KUFIKA MAHAKAMANI KUTOA USHAHIDI
NA FATMA HAMAD - PEMBA
Ucheleshwaji wa uendeshwaji wa kesi
mahakamani ni chanzo kinachochangia baadhi ya wananchi kushindwa kufika
mahakamani kutoa ushahidi katika kesi za udhalilishaji hali ambayo inapelekea
kesi hizo kushindwa kupata hukumu na hatimae hupelekea kufutwa.
Wakizungumza katika mkutano wa majadiliano juu ya kupambana na
udhalilishaji wa kijinsia, wananchi wa mkoa wa kusini pemba katika mkutano ambao umewakutanisha watumishi mbali mbali wa
Serikali wakiwemo mahakimu, madpp, mapolisi, mafias ustawi wa jamii pamoja na
wasaidizi wa sheria huko ukumbi wa chama cha wandishi wa habari wanawake
Tanzania Tamwa Chake chake Pemba.
Wamesema bado uwendeshwaji wa kesi
mahakamani unaonekana kusua sua, hivyo hupelekea wazazi wa wahanga wa matukio ya udhalilishaji kukata tama na
kukataa moja kwa moja kwenda mahakamani kutoa ushahidi.
‘’Ukienda leo unaambiwa mjoo, kesho
ukija unaambiwa kesho kutwa hii inatuumiza hatuna nauli za kila siku, wakati
hata nauli hatupewi mahakamani ni bora
tusamehe tu ‘’Walisema wananchi’’.
Hivyo wamewataka wahusika wa vyombo
vya kisheria kuzipa kipaombele kesi hizo na
kuziendesha kwa haraka ili ziweze
kupatiwa huku jambo ambalo litasaidia kuondosha unyama huo ambao umekuwa ni
hatari kwa Watoto.
Kaimu mrajis wa mahkama kuu chake
chake Abdul Razak Abdul Kadir Ali amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuumwa na tatizo
la udhalilishaji imeanzisha mahakama maalu na kuajiri mahakimu 13 Visiwani
Zanzibar ambapo kwa pemba kuna makimu wa 5 ambao watashuhulikia kesi hizo za udhalilishaji tu ili kupunguza malalamiko
hayo ya mrundikano wa makesi mahakani.
Kwa upande mwengine Abdul razak
amekiri suala la kutokulipwa nauli kwa mashahidi kutokana na ufinyu wa pesa wanayoletewa kutoka Serikali kuu.
Kwa upande wake mratibu wa chama cha
wandishi wa habari wanawake Tanzania Fathiya Mussa Said amesema lengo la
mkutano huo ni kujadiliana changamoto mbali mbali katika zinazo wakabili
watumishi hao katika ufuatiliaji wa kesi za udhalilishaji.
,
Comments
Post a Comment