AFUNGWA JELA KWA KUTOROSHA MSICHANA
Hatimae
kijana Ramadhan Khamis Mohd mwenye umri wa miaka 19 mkazi wa Tironi Mkoani Pemba anza maisha
mapya
ya kutumikia chuo cha Mafunzo kwa muda
wa miaka 5 baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kutorosha
msichana wa miaka
16.
Baada ya
kijana huyo kupanda kizimbani na kusubiri asomewe hukumu yake Mwendesha
mashtaka wa Serikali Mussa Khamis
amemuambia hakimu anaendesha kesi hiyo
kuwa kesi iko kwa ajili ya kutolewa uwamuzi hivyo wao hawana pingamizi kama
mtuhumiwa yuko tayari basi asomewe huku yake.
‘’Kama
mtuhumiwa yuko tayari basi na sisi hatuna tatizo nivyema asomewe hukumu yake ili ajue hatma yake’’
alieleza DPP Mussa.
Hakimu wa
mahakama ya mkoa B iliyopo Chake
chake Muumin Ali Juma
alisema jumla ya mashahidi 4 walisikilizwa
mahakamani hapo akiwemo muathirika mwenyewe na Mahakama imemtia hatiani
mtuhumiwa huyo.
Hivyo kwa
mujibu wa kifungu cha 113 [1] [a] cha sharia ya adhabu namba 6
na kifungu cha
299 cha sharia ya mwenendo wa makosa ya jinai sharia namba 7
za mwaka 2018 sheria za Zanzibar kijana
huyo atatumikia chuo cha Mafunzo kwa muda wa
miaka 5.
Imedaiwa
mahakamani hapo siku ya tarehe 16/1/
2021 majira ya saa 1;30 za usiku huko
Tironi wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba Kijana huyo bila ya halali na bila ya ridhaa ya wazazi wake alimtorosha
msichana wa miaka 16 kutoka nyumbani kwao na kumpeleka katika
geto la Yakuob Abdala Juma hapo
hapo tironi jambo
ambalo ni kosa kisheria.
Comments
Post a Comment