KIRARE BADO AISOTEA RUMANDE
Mahakama ya
mkoa B iliopo Kusini Pemba imeghairisha kesi
ya kuingilia
kinyume na maumbile inayomkabili kijana
Khamis Abdala
Khamis marufu kirare mwenye umri wa
[20] mkaazi
wa Kangani wilaya ya Mkoani baada ya
mtuhumiwa
huyo kukataa kusomewa shitaka lake .
Kijana huyo
wakati akiwa ametulia kizimbani na kusubiri
asomewe
shitaka lake aliambia mahakama hiyo kuwa hali
yake sio mzuri
anaomba kesi ighairishwe na ipangiwe siku
nyengine.
‘’Mheshimiwa
hakimu leo naumwa siwezi kukakaa hivyo
naiomba
mahakama yako ighairishe shauri hilo kwa leo’’
alieleza
mtuhumiwa kirare.
Hakimu wa
mahakama hiyo Muumin Ali Juma amesema hii
ni mara ya pili unasema unaumwa daktari
anakuja na kurudi ila ujue baadae fursa hii hutoipata tena nitakua sikusikilizi
tena , na mahakama itatoa oda ya kumruhusu daktari afanye shughuli zake mpaka
utakapo kuwa tayari ndio tutamleta na
wewe utarudi rumande hadi tarehe 9/ 8
2022kwa ajili ya kusikiliza mashahidi.
Mtuhumiwa
huyo alitenda kosa hilo siku ya rehe 28/ 5/2022 ya
smbili za
usiku huko kangani Sokoni wilaya ya Mkoani bila ya
halali na
bila ya ridhaa ya walezi wake alimtorosha Mtoto wa
miaka 10
kutoka sokoni alipokua amekaa na kumpeleka
kwenye banda
ambalo anaishi, na siku hiyo hiyo wakati wa 2;
7 usiku
ulimuingilia kinyume na maumbile ambapo kufanya
hivyo ni kosa kinyume na kifungu cha 115 cha sharia namba 6 / 2018 sheria ya Zanzibar.
Comments
Post a Comment