mbunge wa wawi aekeza kwenye sekta ya michezo

 



NA FATMA HAMAD FAKI.

Uwanja wa mpira wa miguu  wa  mtega  uliopo  Wilaya ya Chake Mkoa wa kusini Pemba  umeanza kufanyiwa  matengenezo  ili  kuona  unachezeka na unatumika muda  wote.

Akizungumza na wandishi wa habari  mbele ya ukarabati  huo  Mbunge wa jimbo la Wawi Khamis  Kassim   Ali kupitia chama cha Mapinduzi   Amesema  takribani   miaka 45  uwanja  huo  umeonekana  kuchakaa  hivyo  ameamua  kufanyia  ukarabati   ili uwe uwanja   ambao  unaendana  kimichezo.

‘’Nimeamua kutengeneza uwanja huu ili kuwaondoshea changamoto  vijana ambao wameamua kuwekeza katika michezo’’ alieleza mbunge.

Hivyo  Ametaka  wanamichezo hao  kuutunza  na kuulinda  uwanja huo  ambao utaleta manufaa kwao na kwa kizazi chao.

Aidha  mbunge huyo  amesema  suala la mpira  kwa  sasa ni ajira,   hivyo ni wakati vijana kuchangamkia fursa hiyo  kwani kutawawezesha  kujipatia  kipato.


 

kwa upande wake katibu wa timu ya Wawi star  Juma Muhammed Tamimu  amesema mategemeo  yao  ni kuona kwamba uwanja wao umekuwa  uwanja wa kisasa  kama ilivyo viwanja vyengine.

Hichi ni kiwanja cha nne kufanyiwa ukarabati  na mbunge huyo ikiwa ni pamoja na kiwanja cha ndugu kitu, Gombani ya kale na  Nyungu nyungu .

 

 



Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.