WEZI WA KARAFUU WATAKIONA MKUU WA MKOA ASEMA

 



NA FATMA HAMAD PEMBA.


Serikali ya mkoa wa Kaskazini Pemba kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama  mkoani humo imesema hawatomvumilia mtu yoyote atakaefanya  vitendo vya  uhujumu   wa zao  la karafuu katika msimu  wa mwaka huu.

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya micheweni Mgeni Khatib Yahya  kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Kaskazini pemba Salama Mbarouk Khatibu  mbele ya Masheha pamoja na wakulima wa  karafuu mkoa huo  huko jamuhuri Holl Wete Pemba.

Amesema  wakati wa msimu wa karafuu  wapo watu  wanafanya ubabaishaji ikiwemo ununuaji  karafuu za vikombe  pamoja na uzwaji  wa karafuu chafu katika vituo vya ZSTC.

‘’Niwambie wezee wenzangu haipendezi kuonekana kwamba karafuu inanunuliwa na mchanganyiko wa uchafu tunaona aibu kama sisi viongozi, hivyo kwa msimu huu hatutokua tayari kuliona hilo tutahakikisha tumewafichua wote watakaofanya hivyo’’ alieleza mkuu wa mkoa.

Wakitoa changamoto  ambazo zimekua  zikiwaumiza  wakulima hao ni kuzuka kwa wizi na ukatwaji wa mikarauu kwenye mashamba yao.

‘’Mheshimiwa mkuu wa mkowa kwa kweli tunakilio wizi wanatumaliza na hawa wanaonunuwa karafu za vikombe ndio wanaosababisha huu wizi’’ walieleza kwa masikitiko wakulima hao.

Aidha kwa upande mwengine  waliwasisitiza watendaji wa shirika la biashara la ZSTC  kuwa wadilifu wakati wa majukumu yao hususan kipindi cha msimu jambo ambalo litaondosha malalamiko kwa wakulima hao.


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.