HAKIMU AKATAA OMBI LA MBAKAJI.

 


NA FATMA HAMAD PEMBA.


Mtuhumiwa  wa  kesi  ya  ubakaji   Mosi  Othman  Mosi   mkazi wa  Mchakwe  Muambe  ameiomba  Mahakama  kumfutia  shitaka  lake  kwa vile  shahidi ambae ndio muathirika  mwenyewe kushindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi.

‘’tarehe iliyopita   shahidi huyo hakuja,  na leo hakuja  basi muheshimiwa hakimu bora kesi ifutwe ili nirudi zangu kijijini niendelee na maisha yangu’’ alieleza mtuhumiwa mosi.

Hakimu wa mahakama maalumu inayoshuhulikia kesi za ushalilishaji Mkoa wa kusini Pemba Mumin Ali Juma alikataa ombi la mtuhumiwa huyo na kumuambia kuwa kesi hiyo hawezi kuifuta, kwani kuna muda malumu uliowekwa kisheria kama mashahidi hawakuja ifutwe ila hiyo haijafikia muda wa kufutwa.

‘’Si kiubaliani na ombi hilo na kama shahidi huyo hakupatikana basi naomba aitwe shahidi mwengine ili tuweze kusikiliza kesi’’ alisema hakimu Muumin.

Mtuhumiwa Mosi Othman Mosi utaendelea kukaa rumande na utarudi tena mahakamani hapa  tarehe 26/7/2022 kwa ajili ya kusikiliza kesi.

Imedaiwa mahakiamani hapo mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo siku na tarehe isiyofahamika katika mwezi wa julai maka 2018 majira ya kumi usiku huko mchakwe Muambe wilaya ya mkoani mkoa wa Kusini Pemba ulimbaka msichana wa miaka 15 ambapo kufanya hivyo ni kosa kinyume na  kifungu cha 108(1),(2)(e) na 109(1) sheria ya adhabu, Sheria namba 6 ya mwaka 2018, Sheria ya Zanzibar.


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.