VIONGOZI DINI WAPEWA DAWA YA KUMALIZA MIGOGORO

 



 
NA FATMA HAMAD PEMBA.

Viongozi  wa  dini  wametakiwa  kuwa  mstari  wa  mbele  kuwaelimisha  Wananchi   juu ya kulipa paumbele suala  zima la mirathi  jambo  ambalo  litapunguza  migogoro  katika  Jamii.

Ushauri huo umetolewa na wadau waliopata mafunzo juu ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya amani katika kongamano la jenga amani yetu lililoandaliwa na shirika la Seach for Comman Ground lililofanyika Mgogoni Chake chake Pemba.

Wamesema kuwa migogoro ya ardhi ndio tatizo kubwa ambalo linaonekana kuota mzizi  katika familia nyingi hapa Visiwani.

Wameeleza kuwa  familia nyingi hazina tamaduni ya kurithishana mali wanazoachiwa na wazazi wao pindi wanapofariki kitu ambacho ndicho kinachochochea  kuongezeka  kwa migogoro  ya  ardhi  ndani ya Jamii.

‘’Kwa keli tunatatizo tusifichane  hatuna tabia ya kurithishana, na hiyo inapelekea wengine  kukosa haki yao stahiki, hivyo nyinyi mashekha munadhima kubwa  ya kutoa elimu juu ya hilo’’ walieleza wadau wa amani.

Aidha wadau hao wameliomba shirika la Seach for Comman Graund kuendelea kutoa elimu juu ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya mazungumzo jambo ambalo litaepusha uvunjifu wa Amani Nchini.

Kongamano hilo linalohusu  umuhimu wa kutatua migogoro kwanjia ya Amani liliwakutanisha  watu mbali mbali wakiwemo Masheha, Viongozi wa dini, Wanasiasa, Wanahjarakati pamoja na wandishi wa habar.






 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.