OFISI YA MUFTI YA NENA JUU YA WATU WENYE ULEMAVU.


NA FATMA HAMAD FAKI.

Waumini wa dini ya kiislamu pamoja na watu wenye uwezo wa Kusaidia misaada mbalimbali ya kijamii wamehimizwa kuendele  kuwasaidia  wanyonge  hususan  jamii ya watu wenye ulemavu.

Kauli hiyo imetolewa na naibu katibu mufti ofisi ya Pemba Said Ahmad mara baada ya kumtembelea mwalimu wa madrsatul juhudia Sada Khamis Hamad mwenye ulemavu wa viungo mkazi wa Shumba vyamboni wilaya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Alisema ziara hiyo ya kumtembelea mwalimu huyo imekuja kufuatia tarifa iliyotolewa na vyombo vya habari ikiwemo mtandao wa Pemba Ya Leo  Blog iliyonesha changamoto zinazo mkabili mwalimu huyo ya ukosefu wa madrsa ya kufundishia wanafunzi wake.

‘’Kama ofisi ya mufti tumeguswa na hilo na ndio mana tukaamua kuja kukuona na sisi tuweze kukusikiliza kero zako ambazo zinakukabili katika madrasa yako’’ alisema sheikh Said.

Alisema kwa vile ofisi ya mufti ndio mlezi mkuu wa madrsa zote za quran watafanya jitihada mbali mbali pamoja na kutafuta wahisani ili kuona amejengewa madrasa yake jampo  ambalo litatoa hamasa  ya ufundishaji kwa mwalimu huyo.

Alisema   jambo analolifanya  mwalimu huyo wakike la  kufundisha quran ni jambo la kuigwa na  la kupigiwa mfano  hivyo ni vyema  jamii  kumuunga mkono kwa kumsaidia kwa misaada ya hali na mali ili aweze kuendeleza  madrasa yake kwa maslahi ya makubwa ya watoto na jamii kwa upana wake.

Akizungumza mbele ya ugeni huo mwalimu huyo alisema kuwa changamoto kubwa inayomkabili katika madrasa yake ni ukosefu wa sehemu salama ya kufundishia.

‘’Hapa barazani ninaposomeshea panavuja mvua ikinyesha hatakama ni siku tatu wanafunzi hulazimika kubaki nyumbani mpaka pale mvua itakapo pita’’ alieleza mwalimu.

Nao wanafunzi wanasoma katika madrasa hiyo waliufurahia ugeni huo wakisema wamepata matumaini  kwamba utakua ni muarubaini wa kupata ufumbuzi changa moto hiyo inayowakabili madrasani hapo.




 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.