MTUHUMIWA AKATAA SHITAKA

 NA FATMA HAMAD PEMBA.

Mahakama  ya  mkoa B iliopo   Kusini Pemba  imeghairisha  kesi ya  kuingilia kinyume na maumbile   inayomkabili   kijana  Khamis  Abdala Khamis  marufu   kirare   mwenye  umri   wa   [20] mkaazi  wa  Kangani  wilaya ya Mkoani   baada ya mtuhumiwa huyo  kukataa kusomewa shitaka lake .

  Kijana  huyo wakati akiwa  ametulia  kizimbani  na  kusubiri  asomewe  shitaka  lake  aliambia mahakama  hiyo kuwa hali yake sio mzuri  anaomba  kesi ighairishwe na ipangiwe  siku nyengine. 

‘’Mheshimiwa hakimu leo naumwa   siwezi kukakaa hivyo  naiomba mahakama yako  ighairishe shauri  hilo kwa leo’’ alieleza  mtuhumiwa  kirare.

Hakimu wa mahakama hiyo  Muumin  Ali  Juma hakufurahishwa na kauli  hiyo  na kumueleza   mtuhumiwa  huyo  kwamba  hiyo ni haki yako  na inahitajika upewe.

 Lakini tu  nikueleze  leo  shahidi  ambae  ni  daktari  amekuja wewe unasema unaumwa  ila  na siku akidharurika  yeye  tutamruhusu aende na safari zake utaendelea  kukaa ndani atakapo rudi.

‘’ Usije ukasema  mimi nitafuta  kesi  la hasha  hilo  sifanyi  katu unajichelewesha  mwenyeo  utaendelea kukaa ndani’’ alieleza kwa msisitizo hakimu  Mumin.

Na kesi hii itarudi tena mahakamani  hapa siku ya tarehe  27/7/ 2022 kwa ajili ya kusikilizwa.

Mtuhumiwa  huyo alitenda kosa hilo siku ya rehe 28/ 5/2022 ya smbili za usiku  huko kangani Sokoni  wilaya ya Mkoani  bila ya halali na bila ya ridhaa ya walezi wake  alimtorosha  Mtoto wa miaka 10  kutoka sokoni alipokua amekaa na kumpeleka  kwenye banda ambalo anaishi,  na siku hiyo  hiyo  wakati wa  2; 7 usiku ulimuingilia  kinyume  na  maumbile  ambapo  kufanya hivyo  ni  kosa  kinyume na kifungu cha 115 cha sharia namba 6 ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar.


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.