ALIEDAIWA KUWA NI BUBU SASA AANZA KUSEMA
Hatimae Mahakama
ya mkoa B
Wete yanza kusikiliza kesi ya
ulawiti inayomkabili kijana Nuhu Kombo
Nuhu miaka 19 mkaazi wa Kijichame wilaya ya Micheweni mkoa
wa Kaskazini Pemba.
Mwendesha
mashtaka wa Serikali Juma Mussa Omar amemuambia hakimu anaendesha kesi hiyo kuwa shauri hilo lipo kwa ajili ya
kusikilizwa na tulikua tunasubiri
cheti kutoka kwa mtaalamu wa Afya
kuthibitisha kwamba kijana huyo ni mgonjwa hawezi kuzunguza ama ni kiziwi.
‘’Mheshimiwa
hakimu tulitoa ombi mahakama yako
impeleke hospitali kwa ajili ya
kufanyiwa uchunguzi kama tayari basi
tupo tayari kwa ajili ya kuskila’’ alisema DPP Juma.
Hakimu
wa Mahakama hiyo Abdulrahman Ali
ameleza kuwa tayari tumesha pokea uthibitisho kutoka Hospitali na majibu hayakuonesha kwamba mtuhumiwa huyo ana ugonjwa
wowote.
‘’Majibu
yanaonesha kwamba si kibubu wala kiziwi anazungumza hivyo naighairisha hadi
tarehe 25/7 na mashahidi waitwe tuanze
kuwasikiliza’’ alieleza hakimu
Abdulrahman.
Tukio hilo
lilitokea tarehe 13/ 12/ 2021 majira ya sa moja asubuhi huko kijichame wilaya
ya Micheweni mkoa wakaskazini Kaskazini
Pemba ambapo mtuhumiwa alimlawiti kijana mwenye ulemavu wa akili.
Ilidaiwa
kuwa kufanya hyivyo ni kosa kinyume na
kifungu cha 116[1] cha sheria nambari 6/2018 sheria ya Zanzibar.
Comments
Post a Comment