WAKULIMA WA KARAFUU MKOANI PEMBA WA NENA.

 



NA FATMA HAMAD PEMBA.

Wakulima wa zao la karafuu  wilaya ya Mkoani wameliomba shirika  la biashara la ZSTC  kuweka mikakati madhubuti  ili waweze kuwadhibiti wale wote  wanao jishuhulisha na biashara ya  ununuzi wa  karafuu   mbichi. 

Wamesema uwepo wa watu wanao nunua karafuu mbichi za vikombe ni moja  ya sababu kubwa inayochangia  ongezeko la wizi  wa  zao hilo.

Ushauri huo wameutoa katika mkutano wa  tathmini juu ya zao la karafuu katika msimu  wa mwaka huu huko Zstc Mkoani wamesema asilimia kubwa ya wanaoiba karafuu wanaziuza kwa wale wanao nunua karafu za vikombe, hivyo ni vyema watendaji wa Zstc kuwa makini na watu hao ili kuepusha uharibifu, pamoja na wizi  katika msimu wa mwaka huu.

‘’Mheshimiwa mkuu wa mkoa kweli tunaumizwa tunaibiwa karafuu zetu na hawa wanunuzi wa karafuu za vikombe ndio wanaosababisha tunaomba hilo mliangalie’’ walieleza wakulima.

Kwa upande wake mkulima Zubeir Mohd Said amesema  sababu inayowapelekea wakulima kuuza karafuu mbichi ni ule ucheleweshwaji wa muda  wa kuanza  kununua  katika vituo vya Zstc.

Mapema mkuu wa mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor  Masoud amewatoa hofu wakulima hao na kuwambia kua wataendelea kutoa  adhabu  kali dhidi ya wale  wote watakao fanya vitendo vya uharibifu wa zao la karafuu  ambavyo vinapelekea uhujumu uchumi wa Nchi pamoja na wazalishaji.

Akitoa tathmini ya utekelezaji wa zao la karafuu kwa mwaka 2021-2022  kaimu mkurugenzi mwendeshaji wa shirika la  Zstc  Zanzibar  Ali  Suleiman Mussa  amesema jumla ya tani Elfu nane  mia  tano  na  sita nukta  tatu Sifuri  zilinunuliwa na shirika hapa kisiwani Pemba katika msimu uliopita.


Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.