JAMII YAHINIZWA KUITUNZA AMANI

 

NA FATMA HAMAD PEMBA.

Wadau  wa   ujenzi   wa   Amani  Kisiwani Pemba wametakiwa  kuendelea   kuielimisha jamii  juu   ya  athari   za  migogororo    na weweze   kujiepusha  ndani   ya   familia   zao.

Wito huo umetolewa na Afisa mdhamini ofisi ya rais tawala za mikoa na idara malum za SMZ  wakati akizungumza na wadau waliopatiwa  taluma ya  ujenzi wa amani huko  Green Folage Hotel iliyopo Chake chake  Mkoa wa Kusini Pemba.

Amesema amani ndio msingi mkuu unaosababisha  maendeleo  Nchini, hivyo ni wakati  kwa kila  mtu kwa anafasi yake  kuchukua hatua ya kuwaelimisha wenzake  kuepuka kufanya mambo ambayo yanapelekea  migongano na mifarakano  isiyoyalima.

‘’Wadau  wenzangu  bado tunajukumu kubwa la kuisaidia jamii  kuwafahamisha jinsi ya kutatuwa  migogoro  kwa njia  ya  amani ili  kuona wanaishi kwa  kuvumiliana  na kusameheana  bila ya kulipiziana visasi ’’ alieleza Ofisa mdamini.

Aidha kwa upande mwengine amewataka  wananchi  kutoa mashirikiano ya hali ya juu  na kushiriki  kikamilifu   zoeze la Sensa ambalo linatarajiwa kufanyika   mwezi wa nane mwaka huu 2022.

 Nao Washiriki wa mkutano huo wamesema  dawa kubwa ya kumaliza migogoro  ni kuhakikisha kila mmoja mwenye dhamana au cheo flani  atekeleze  majukumu yake kwa misingi yake inavyomuelekeza  bila ya kuonesha ubaguzi wakati wa tekelezaji  wa majukumu yake.

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.