NUHU AENDELEA KULA BATA RUMANDE

 


NA FATMA HAMAD Pemba. 

Mahakama  ya mkoa  B iliyopo  Wete  imeghairisha  shauri  la  Ulawiti  linalo mkabili  kijana  Nuhu Kombo  Nuhu  mwenye  umri  wa  miaka 19  mkazi  wa  Kijichame  wilaya  ya  Micheweni  Mkoa  wa Kaskazini  Pemba baada ya mtuhumiwa kudai  kuwa anaumwa na homa.

Mtuhumiwa huyo   ameiambia mahakama hiyo kuwa hajisikii vizuri anaumwa hivyo anaiomba  kughairisha shauri hilo na apangiwe siku nyengine kwa ajili ya kusikilizwa.

Mwenedesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka DPP Juma Mussa Omar  amewambia mashahidi waliofika kwa ajili ya kutoa  ushahidi  wao kwamba mtuhumiwa leyo kasema anaumwa hivyo tukiendelea  tutakua tunamnyima haki yake .

‘’Kwa vile mtuhumiwa kasema hayuko vizuri nawaomba murudi na musichoke muje tena siku mutakayoitwa’’ alieleza DPP Juma.

Hakimu wa mahakama hiyo amekubaliana na ombi hilo nan a kusema kuwa mtuhumiwa  atarudi rumande hadi siku ya tarehe 3/ 8/ 2022 kwa ajili ya kusikiliza mashahidi.

Tukio hilo lilitokea tarehe 13/ 12/ 2021 majira ya sa moja asubuhi huko kijichame wilaya ya Micheweni mkoa wakaskazini  Kaskazini Pemba ambapo mtuhumiwa alimlawiti kijana mwenye ulemavu wa akili.

Ilidaiwa kuwa kufanya hyivyo ni kosa  kinyume na kifungu cha 116[1] cha sheria nambari 6/2018 sheria  ya Zanzibar.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTELEKEZAJI WA WANAWAKE UNAVYOKATISHA NDOTO ZA WATOTO.

Mkuu wa Polisi Jamii Kaskazini Pemba akerwa na wanao wafungia ndani watoto wenye ulemavu.

Mrajisi wa Mahakama Zanzibar ahidi kula sahani moja na Mahakimu wasio wadilifu.