Naibu Chauma asema: ‘’Chagueni viongozi wenye imani na Nchi yao’’
NA FATMA HAMAD, PEMBA Wananchi wametakiwa kuwachagua viongozi ambao wanauthubu na wenye uzalendo na nchi yao, wanaoweza kusimama na kutetea shida zinazowakwaza wananchi wao. Kauli hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma Chauma Zanzibar, Mohamed Masoud Rashid wakati akizungumza na wanachama na wananchi wa chama cha Chauma, katika uzinduzi wa kampeni za wagombea wa Ubunge, Uwakilishi na Udiwani huko Tumbe wilaya ya Micheweni kisiwani Pemba. Alisema wakati umepita wa kuchagua viongozi kwa ajili ya chama ama kwa cheo chake, bali ni vyema kuhakikisha wanawachagua ambao wanauchungu na nchi yao na wanauwezo wa kutetea kero za wananchi, sambamba na kuwaletea mabadiliko. ‘’Nduguzangu wanatumbe badilikeni msichague viongozi ambao hawana maendeleo, isiwe wanaishia kupiga kofi tu kwenye meza,’’alisema. Aidha alisema endapo chama chao kitaingia madarakani, jambo la kwanza watakalolifanya ni kushusha bei za vyakula, ili kuona kila mwananc...